Tuesday 17 March 2015

Kipa Vicent Enyeama kudaka mechi ya 100


Kipa Vicent Enyeama akitengeneza sosi lake.

ABUJA, Nigeria
KIPA wa Nigeria Vincent Enyeama anajiandaa kucheza mchezo wake wa 100 wa kimataifa baada ya kutangazwa katika kikosi cha Super Eagles kitakachocheza mchezo wa kirafiki na Bolivia utakaofanyika Machi 26.

Enyeama mwenye umri wa miaka 32 ni miongoni mwa wachezaji 28 waliochaguliwa kuunda kikosi hicho kilichopo chini ya kocha wa muda Daniel Amokachi.

Mshambuliaji aliye katika fomu wa West Brom, Brown Ideye naye yumo katika kikosi hicho, pamoja na Odion Ighalo wa timu ya daraja la kwanza ya Watford.

Mshambuliaji majeruhi wa Stoke Victor Moses naye pia yuko katika skwadi hiyo ambaye amemuhakiishia kocha Amokachi kuwa atakuwa fiti kucheza mchezo huo.

Kikosi hicho cha timu ya taifa ya Nigeria kitakuwa pamoja na kusafiri kwenda Afrika Kusini kucheza mchezo mwingine wa kirafiki Jumapili, Machi 29.

Kikosi Kamili cha Nigeria:
Makipa: Vincent Enyeama (Lille OSC, Ufaransa); Theophilus Afelokhai (Kano Pillars); Chidiebere Eze (Ifeanyi Ubah United)

Mabeki: Chima Akas (Sharks FC); Godfrey Oboabona (Rizespor FC, Uturuki); Azubuike Egwuekwe (Warri Wolves); Nelson Ogbonnaya (Heartland FC); Kenneth Omeruo (Middlesbrough FC, England); Akeem Latifu (Aalesunds FC, Norway); Leon Balogun (Darmstadt 98, Ujerumani).

Viungo: Ogenyi Onazi (SS Lazio, Italia); Steven Ukoh (Biel-Bienne FC, Uswisi); Sone Aluko (Hull City, England); Hope Akpan (Reading FC, England); John Ogu (Hapoel Be'er Sheva, Israel); Michael Babatunde (Volyn Lutsk, Ukraine); Joseph Nathaniel (Sharks FC); Kingsley Sokari (Enyimba FC).

Washambuliaji: Ahmed Musa (CSKA Moscow, Russia); Aaron Samuel (Guangzhou R&F, China); Brown Ideye (West Brom, England); Odion Ighalo (Watford FC, England); Anthony Ujah (FC Cologne, Ujerumani); Moses Simon (KAA Gent, Ubelgiji); Ubong Moses (Kano Pillars); Stanley Dimgba (Warri Wolves); Mfon Udoh (Enyimba FC); Standby - Victor Moses (Stoke City, England)

No comments:

Post a Comment