Saturday 7 March 2015

Wawili wakamatwa wakituhumiwa kumuua mpinzani Russia



MOSCOW, Russia
WANAUME wawili wanashikiliwa na vyombo vya usalama kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya mwanasiasa wa upinzani wa Russia Boris Nemtsov, taarifa kutoka Makao Makuu ya Usalama (FSB) imeeleza.

Anzor Gubashev na Zaur Dadayev, wote kutoka mkoa wa Caucasus, walikamatwa Jumamosi, alisema mkurugenzi wa FSB Alexander Bortnikov.

Wapelelezi wa Russia walisema kulikuwa na mipango ya kufanya mauaji hayo.

Mauaji hayo katika eneo maarufu la darajani ndani ya eneo hilo la kiistoria la Kremlin yalishtua Russia.

Naibu Waziri Mkuu wazamani na mwasiasa mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 55, alipigwa risasi mgongoni mara nne usiku wa Februari 27 wakati akitembea mtaani na rafiki yake wakike.
Mwanasiasa huyo alizikwa Jumanne jijini hapa.

Taarifa hiyo imetolewa na televisheni ya taifa na mkuu wa FSB mwenyewe ikiwa ni alama ya wazi kuwa Kremlin anataka kuonekana akilichukulia jambo hilo kwa makini zaidi.

Bwana Bortnikov hakutoa taarifa zaidi jinsi watuhumiwa hao wanayoshikiliwa, katika taarifa yake fupi iliyotolewa na televisheni inayomilikiwa na taifa ya Channel One, lakini alisema kuwa uchuguzi ulikuwa bado unaendelea.

No comments:

Post a Comment