LONDON, England
KLABU ya Sunderland imemtupia virago kocha wake Gus
Poyet baada ya kuiwezesha timu hiyo kushinda mchezo mmoja tu kati ya 12 ya Ligi
Kuu ya England inayoendelea.
Timu hiyo inayojulikana pia kama Paka Weusi iko pointi
moja juu ya ukanda wa kushuka daraja baada ya Jumamosi kupokea kipigo cha mbwa
mwizi cha bao -0 kutoka kwa Aston Villa tena kwenye uwanja wao wa nyumbani.
"Uzuni, hatujaweza kupiga hatua yoyote
iliyotegemewa na hata mmoja wetu msimu huu, “ alisema mwenyekiti wa
klabu hiyo Ellis Short.
"Tunajikuta tukipambana, kwa mara nyingie tena, hatimaye
tutakuwa na mwisho mbaya chini ya msimamo wa ligi. Tumefanya uamuzi mgumu ambao
ulikuwa ukihitajika kwa ajili ya mabadiliko.”
Taarifa hiyo ya Sunderland iliendelea kueleza kuhusu
mbadala wa Poyet atakayechukua mikoba ya kocha huyo.
Timu hiyo Jumamosi itakuwa na safari ya kwenda West Ham
kabla ya kucheza na wapinzani wake wa mji Newcastle Aprili 5 mwaka huu.
Poyet, 47, Jumatatu alikuwa na mazoezi na wachwzaji wa
timu hiyo asubuhi lakini baadae alikutana na Mtendaji Mkuu Margaret Byrne na
wajumbe wengine wa bodi kujua hatma yake.
Poyet aliichukua timu hiyo kutoka kwa Paolo Di Canio Oktoba
mwaka 2013 klabu ikiwa mkiani mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England.
Lakini baada ya sare nne kutoka katika mechi zao sita
za mwisho, iliisaidia timu hiyo kukwepa janga la kushuka daraja.
No comments:
Post a Comment