Friday 20 March 2015

Fainali Ligi ya Mabingwa wa Ulaya kujirudia msimu huu



LONDON, England
MABINGWA watetezi Real Madrid watakutana na wapinzani wao wa jiji Atletico Madrid katika mchezo war obo fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya, ikiwa ni marudio ya fainali ya msimu uliopita.

Timu ya Ufaransa ya Paris St-Germain ambayo iliifunga Chelsea katika hatua ya 16 bora itakuwa na kibarua kigumu pale itakapocheza na Barcelona, ambayo iliwafunga mabingwa wa Ligi Kuu ya England Manchester City.

Monaco, iliyoifungisha virago Arsenal kwa faida ya bao la ugenini, imepangiwa kucheza na Juventus, wakati mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich watakabiliana na Porto.

Mechi za kwanza za hatua hiyo ya robo fainali zitapigwa kati ya Aprili 14-15 April, huku mapambano ya marudiano yatachezwa Aprili 21-22.

Real Madrid ilitwaa taji lake la 10 la Ulaya baada ya kuwafunga katika fainali mabingwa wa Hispania  Atletico kwa bao 4-1 katika muda wa nyongeza katika mchezo uliochezwa Lisbon nchini Ureno msimu uliopita.

Ratiba Kamili:

Paris St-Germain v Barcelona

Atletico Madrid v Real Madrid

Porto v Bayern Munich

 Juventus v Monaco

TAREHE ZA ROBO FAINALI:

Aprili 14: - Atletico Madrid vs Real Madrid, Juventus vs Monaco

Aprili 15: - PSG vs Barcelona, Porto vs Bayern Munich 

Aprili 21: Barcelona vs PSG, Bayern Munich vs Porto


Aprili 22: - Real Madrid vs Atletico Madrid, Monaco vs Juventus

Head-to-head 

PARIS SAINT-GERMAIN 

Walizifunga timu gani hadi kufikia hatua hii?

PSG ilimaliza ya pili katika kundi la F nyuma ya vinara Barcelona,ikishinda mara nne katika mechi zake, ikitoka sare na Ajax na kufungwa na Barca. Walicheza na Chelsea katika hatua ya 16 bora, ambapo walitoka 1-1 katika mchezo wa kwanza kabla ya kutoka sare ya 2-2 huku ikibaki na wachezaji 10 katika mchezo wa marudiano jijini London.
Kocha

Laurent Blanc

Mfungaji anayeongoza kwa mabao:
Edinson Cavani - 6

Wamewahi kutwaa taji hilo?

Hapana.

 
BARCELONA

Walizifunga timu gani hadi kufika hapa?:

Barcelona walimaliza kileleni katika Kundi F, wakishinda mechi tano kati ya mechi zao walizocheza na walipoteza kwa kufungwa 3-2 dhidi ya PSG. Walicheza na Manchester City katika hatua ya 16 bora, wakishinda 2-1 kwenye uwanja wa Etihad na 1-0 kwenye uwanja wao wa Nou Camp.

Walitinga robo fainali kwa ushindi wa jumla ya mabao 3-1.

Kocha

Luis Enrique
Mfungaji anayeongoza kwa mabao
Lionel Messi - 8

Wamewahi kutwaa taji hilo?

Ndio, Mara nne (ushindi wa pili mara tatu)
--
Kukutana:
Timu hizi zimekutana mara mbili kabla ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya. Timu hiyo ya Ufaransa ilisonga mbele kwa ushindi wa jumla ya mabao 3-2 mwaka 1995, wakati Barcelona walisonga mbele kwa faida ya mabao ya ugenini mwaka 2013 (baada ya matokeo ya jumla kuwa 3-3).

    Barcelona haijawahi kushinda mara tatu ugenini walipocheza na PSG (L2 D1), ikiwemo kufungwa 3-2 mwaka huu katika hatua ya mtoano

    PSG ilifugwa mara moja na kutoka sare mara mbili katika ya mechi zao tatu za ugenini walizochezea Nou Camp kukabiliana na Barca, ikiwemo kufungwa 3-1 mwaka huu katika hatua ya makundi.

    Timu zote zimefunga katika mechi sita kati ya saba walizocheza huko nyuma kati ya timu hizo katika mashindano ya Ulaya. Mechi pekee ambayo hakuna timu iliyofunga bao ilikuwa mwaka 1997 katika fainali ya Kombe la Washindi, huku Barcelona ikishinda 1-0.

    Lionel Messi amefunga mabao matatu katika mechi nne za Ligi ya Mabingwa wa Ulaya dhidi ya wapinzani wao hao wa Ufaransa, wakati Neymar pia alifunga katika mechi zote za hatua ya makundu dhidi yao msimu huu.

    Barca imepoteza mchezo mmoja tu kati ya 11 iliyopita dhidi ya wapinzani wao hao wa Ufaransa, na sasa wanakutana tena msimu huu.
-
ATLETICO MADRID 

Walizifunga timu gani hadi kufika hapa?

Atletico walimaliza kileleni mwa msimamo wa Kundi A,
wakishinda mechi nne, wakitoka sare mara moja na Juventus na kushindwa nyingine 3-2 dhidi ya Olympiacos.Walicheza na Bayer Leverkusen katia hatua ya 16 bora, wakifungwa ugenini 1-0 lakini walishinda kwa idadi kama hiyo nyumbani. Walikwenda katika muda wa nyongeza na baadae penati.

Kocha

Diego Simeone

Mfungaji anayeongoza kwa mabao

Mario Mandzukic - 5

Wamewahi kutwaa taji hilo?

Hawajawhi (wamewahi kuwa washindi wa pili)

REAL MADRID 

Baadhi ya wachezaji wa Real Madrid.
Walizifunga timu gani hado kufika hapa?

Real Madrid ilimaliza ya kwanza katika msimamo wa Kundi B, ikishinda mechi zake zote sita dhidi ya Basle, Liverpool na Ludogorets. Walicheza na Schalke katika hatua ya 16 bora, wakiifunga 2-0 huko Ujerumani lakini walifungwa 4-3 huko Madrid. Walisonga mbele katika hatua ya robo fainali kwa ushindi wa jumla ya mabao 5-4.

Kocha
 
Carlo Ancelotti

  Mfungaji bora

Cristiano Ronaldo - 8

Wamewahi kutwaa taji hilo?
Ndio, mara 10 (ushindi wa pili mara tatu).
-
Wamekutana mara ngapi?

    Atletico Madrid na Real Madrid tayari wamekutana mara sita msimu huu huku Atleti ikiwa haijafungwa, ikishinda mara nne (ikiwemo mechi zote mbili za ligi) na kutoka sare mara mbili.

    Atletico Madrid imefunga mara moja katika mechi zote nne walizokutana Ulaya huku wapinzani wake hao wa jadi Real, wakishinda mara moja tu na kushindwa mara tatu.

  Ikiwemo msimu huu, angalau wana uhakika wa kuiwezesha Hispania kuwa na timu moja katika hatua ya robo fainali angalau mara 10 katika kampeni zao.

    Mara ya nne tu katika historia ya mashindano hao ya Ulaya, mchezo wa robo fainali utazikutanisha timu mbili za Hispania; hatahivyo huu ni msimu wa pili mfululizo hilo kutokoea (Real Madrid v Sevilla mwaka 1958 na Atletico v Barcelona mwaka 2014).

PORTO

Walizifunga timu gani hadi kufika hapo?
Porto ilimaliza kileleni katika msimamo wa Kundi H, ikishinda mara nne kati ya mechi zake na kutoka sare mara mbili. Ushindi wao wa kukumbukwa zaidi ule walipoifunga BATE 6-0 katika mchezo wa ufunguzi wa hatua ya makundi. Pia waliwafunga 3-0 ugenini. Walicheza na Basle katia hatua ya 16 bora, walitoka sare ya 1-1 na ugenini kabla ya kushinda 4-0 nyumbani na kupata ushindi wa jumla ya mabao -1.
Kocha
Julen Lopetegui

Mfungaji bora
Jackson Martinez na Yacine Brahimi wote wamefunga 5

Wamewahi kutwaa taji hilo?

Ndio, Mara mbili
BAYERN MUNICH

Walizifunga timu gani hadi kufika hapa?
Bayern walimaliza kileleni katika msimamo wa Kundi E,walishinda mechi tano kati ya mechi walizocheza na kupoteza mara moja dhidi ya Manchester City. Ushindi wao mnono ulikuwa dhidi ya Roma, baada ya kuifunga bao 7-1 huko Italia. Walicheza na Shakhtar Donetsk katika hatua ya 16 bora, walitoka suluhu ugenini lakini walishinda 7-0 nyumbani.
Kocha
Pep Guardiola

Mfungaji bora
Thomas Muller - 5

Wamewahi kutwaa taji?

Ndio mra tano (washindi wa pili mara tano).
Walipokutana
    Bayern ilipoteza mara moja tu kati ya mechi 22 ya mashindano walizokutana dhidi ya timu hiyo ya Ureno (ushindi mara 13, sare nane): fainali ya Kombe la Ulaya mwaka 1987: 1-2 dhidi ya Porto.
    Bayern walishinda katika hatua ya mwisho ya mtoano walipocheza dhidi ya timu hiyo ya Ureno 12-1: 5-0 ugenini na 7-1 nyumbani dhidi ya Sporting katika hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya mwaka 2008/09.
    Ushindi pekee wa Porto katika hatua ya mtoano ya mashindano ya Ulaya dhidi ya timu za ujerumani ulipatikana mwaka 1987 katika fainali; walitolewa katika mechi tatu za mtoano tangu wakati huo, mbili dhidi ya Bayern n moja dhidi ya Schalke.
    Bayern Munich wameshinda mechi saba kati ya tisa walizokutana dhidi ya timu za ureno, kwa ujumla wakifungwa mbili tu.
JUVENTUS

Wamezifunga timu zipi hadi kufika hapa?
Juventus walimaliza wa pili katika Kundi A, wakishinda mechi tatu, wakitoka sare moja na Atletico na wakipoteza nyingine dhidi ya Olympiacos. Walicheza na Borussia Dortmund katika hatua ya 16 bora, wakishinda 2-1 nyumbani na kuwafunga Wajerumani 3-0 ugenini na kushinda kwa jumla ya mabao 5-1.
Kocha
Massimiliano Allegri
Mfungaji anayeongoza
Carlos Tevez - 6

Wamewahi kutwaa taji hilo?

Yes. Mara mbili mara tano wamemaliza wa pili).
MONACO

Wamezifunga timu zipi hadi kufika hapo?
Monaco walimaliza wa kwanza katika Kundi C, wakishinda mechi tatu, wakitoka sare mara mbili dhidi ya Benfica. Walicheza na Arsenal katika hatua ya 16 bora na kuifungasha virago kwa jumla ya bao 3-1 ugenini kabla ya kufungwa 2-0 nyumbani na kusonga mbele.
Kocha
Leonardo Jardim

Mfungaji anayeongoza;
Lucas Ocampos, Aymen Abdennour, Yannick Ferreira-Carrasco, Dimitar Berbatov, Geoffrey Kondogbia, Fabinho, Joao Moutinho wote kila mmoja amefunaji bao moja.

Wamewahi kutwaa taji hilo?

Hawajawahi (wameishia namba mbili).

Mara walizokutana:
   Timu hizo mbili zimekutana mara moja tu kabla ya msimu wa mwaka 97/98 katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya, wakati Juventus waliposhinda 4-1 nyumbani na kupoteza kwa bao 2-3 huko Monte Carlo wakati wakielekwa katika fainali ambako walifungwa 1-0 na Real Madrid.

    Walipokutana na timu za Ufaransa katika mashindano ya Ulaya mara 24 pamoja na timu za Ufaransa (ikiwemo Intertoto), kibibi hicho cha Turin kikipoteza mara tano, kikishinda mara 14 na kutoka sare mara tano.

Hatahivyo katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya, Juve imeshinda mara mbili kati ya sita dhidi ya timu za Ufaransa (moja ilishinda dhidi ya Monaco mwaka 1998 na ilishinda dhidi ya Nantes mwaka 1996).

    Katika mechi za Ulaya walizokutana mara 11 na timu za Italia, Monaco ilishinda mara tatu (sare mara mbili na kufungwa mara sita), ingawa ushindi wa mechi mbili kati ya hizo ulikuja katika mechi zao tatu walizocheza mara ya mwisho na timu hiyo ya Serie A.


No comments:

Post a Comment