Wednesday 11 March 2015

Ajali ya basi na lori Iringa yaua 43


Umati wa watu ukishuhudia ajali hiyo.


Na Mwandishi Wetu, Iringa
WATU 43 wamefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea Iringa baada ya basi la Majinja Express lilikuwa likitokea Mbeya kwenda Dar es Salaam kugongana na lori na kuanguangukiwa na kontena.

Kwa taarifa zilizopatikana katika eneo la tukio, watu 37 walifariki papo hapo na wengine sita walifariki katika hospitali ya Mufindi mkoani Iringa akiwemo mwanafunzi mmoja.

Huzuni kubwa ilitawala katika mji mdogo wa Mafinga baada ya ajali hiyo huku wasamaria wema wakijitahidi kuondoa miili ya waliokufa, na kuwakimbiza hospitalini majeruhi.

Ajali hiyo ilihusisha lori lenye namba T689 APJ likiendeshwa na dereva aliyejulikana kwa jina la Maka Sebastian (26)mali ya CIPEX Company huku basi likiwa na namba T438 CDE likiendesha na dereva Baraka Gabriel (37).

Habari zisizothibitishwa zinasema kuwa mekana wengi wao ni wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliokuwa wakitokea jijini Mbeya kati ya hao walofariki ni wanaume 33 wanawake 7, watoto 3 na majeruhi 22.

Mmoja wa abiria wa basi hilo,Musa Mwasege akisimulia chanzo cha ajali hiyo alisema kuwa chanzo ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa  basi alilopanda kwa kuwa katika mwendo kasi licha ya ubovu wa barabara hiyo kuwa na mashimo mengi yanayosababisha ajali.

Sehemu iliyotokea ajali kwa kweli ni mbovu hivyo dereva wetu baada ya kupunguza mwendo akawa anazidi kuongeza na kutumbukia katika shimo na kusababisha kugongana uso kwa uso na roli hilo na kisha kontena kutuangukia baada ya hapo sikutambua lolote hadi nilipofika hospitali, alisema.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza akizungumza katika eneo la ajali alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni ubovu uliokithiri wa barabara hiyo na ni tukio la kuhuzunisha sana kwa Watanzania na kuagiza wakala wa barabara kuanza matengenezo ya barabara hiyo mara moja.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi, amekiri kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa chanzo cha ajali ni ubovu wa barabara kutokana kuwa na mashimo mengi.

Kamanda Mungi aliwataja abiria waliokuwemo katika basi hilo kuwa ni Esta Emanuel Lusekelo, Jerimiah Wakison, Doto Katuga, Diga Solomon, Theresia Kaminyage, Frank Chiwango,
Luteni Sanga, Alfred Sanga, Juliana Bukuku, Esta Fide na Paulina Justin.

Wengine ni Catherine Mwajengi, Zira Kasambala, Rebeka Kasambala, Mbamba Ipyana, Dulile Kambala, Frank Mbaule, Mustapha Ramadhan, Bwana Mussa, Shadrak Msigwa, Mathias Justin, na mwingine alijulikana kwa jina moja la Elias.

Naye mganga Mkuu Mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya Mufindi Boaz Mnenegwa alikiri kupokea maiti 37 na majeruhi 22 zilizotokana na ajali hiyo na kusema kuwa majeruhi watano walifariki mara baada kufikishwa hospitalini hapo.

Alisema kuwa kutokana ufinyu wa nafasi katika chumba cha kuhifadhia mahiti hospitalini hapo maiti 32 zilipelekwa katia hospitali ya rufaa ya Iringa kwa ajili ya kuhifadhiwa.

No comments:

Post a Comment