Tuesday 10 March 2015

Guadiola ahofia kibarua chake Bayern ikifungwa



MUNICH, Ujerumani
KOCHA wa Bayern Munich Mhispania Pep Guadiola amekiri kuwa hatma ya kibarua chake iko shakani endapo timu hiyo itashindwa kufuzu kucheza robo fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Guardiola alikiri kuwa huenda akapoteza kazi yake endapo Bayern Munich watafungwa na Shakhtar Donetsk katika mchezo wa Jumatano wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Bayern inapewa nafasi kubwa ya kusonga mbele kwa hatua ya robo fainali kufuatia sare ya bila kufungana katika mchezo wa kwanza uliofanyika Ukraine, licha ya kumpoteza mchezaji wao Xabi Alonso aliyetolewa nje.

Hatahivyo, Guardiola ianajua vizuri matarajio ya wapenzi wa timu hiyo katika mchezo utakaofanyika kwenhe uwanja wa Allianz Arena, na anaamini kuwa hata kucheza fainali ya mashindano hayo bado hakumuhakikishii kuendelea kuwepo klabuni hapo.

Alisema wakati wa mkutano wake kabla ya mechi: "Bado mimi ni kijana mdogo, lakini najua nini kitatokea endapo hatutavuka hatua hii na kucheza hatua inayofuata.

"Mimi ni kocha wa klabu kubwa kweli kweli na ninajia ni shida endapo hatutasonga mbele katika robo fainali au nusu fainali, au hata fainali. Hiyo ni sehemu ya kazi yangu na ninajiandaa kwa hilo."

No comments:

Post a Comment