Tuesday 16 February 2016

Tff yatangaza viingilio na waamuzi watakaochezesha mpambano wa Simba na Yanga Jumamosi Uwanja wa Taifa




Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo limetangaza viingilio vya mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) Jumamosi kati ya watani wa jadi Simba SC dhidi ya Yanga SC utakaochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, huku kiingilio cha chini kikiwa ni sh.7,000 tu.

Kiingilio cha juu cha mchezo huo kitakua sh. 30,000,  (20,000) VIP B & C, Elfu Kumi (10,000) kwa viti vya rangi ya machungwa (Orange), na 7,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani.

Tiketi za mchezo huo zitaanza kuuzwa Ijumaa saa 2:00 asubuhi katika vituo vya TFF (Karume), Buguruni Oil com, Ubungo Oilcom, Kidongo Chekundu (Mnazi Mmoja), Posta (Agip), Dar Live (Mbagala), Uwanja wa Taifa, Makumbusho Stand, Kivukoni Ferry.

Mchezo huo utachezeshwa na waamuzi wote wenye beji za FIFA, mwamuzi wa katikati Jonesia Rukyaa (Kagera), akisaidiwa na Josephat Bulali (Tanga), Samwel Mpenzu (Arusha), mwamuzi wa akiba Elly Sasii (Dar) huku Kamisaa wa mchezo huo akiwa Khalid Bitebo (Mwanza).

Ligi hiyo ya Vodacom itaendelea Jumamosi kwa michezo sita, Young Africans v Simba (Taifa), Mbeya City v Azam (Sokoine), Stand United v JKT Ruvu (Kambarage), Toto Africans v Kagera Sugar (CCM Kirumba), Mgambo Shooting v Tanzania Prisons (Mkwakwani) na Majimaji FC v Mtibwa Sugar (Majimaji).

Jumapili ligi hiyo itaendelea kwa michezo miwili, Mwadui FC v Coastal Union uwanja wa Mwadui Complex, huku Ndanda FC wakicheza dhidi ya African Sports uwanja wa Nagwanda Sijaon mjini Mtwara.


Sunday 14 February 2016

Broos ndiye kocha mpya timu ya taifa ya Cameroon


Kocha mpya wa Cameroon, Hugo Broos.

YOUNDE, Cameroon
SHIRIKISHO la Soka la Cameroon (Fecafoot) imemteua mchezaji wazamani wa kimataifa wa Ubelgiji, Hugo Broos, kama kocha mpya wa tembo hao wasiofungika.

Broos, mwenye umri wa 63, amechukua mikoba hiyo kutoka kwa Volker Finke aliyetimuliwa kutoka katika kibarua hicho tangu Oktoba.

Belinga, aliyekuwa kocha wa muda kwa miezi mitatu, atabaki kuwa msaidizi wa Mbelgiji huyo pamoja na mchezaji wazamani wa Ubelgiji, Sven Vandenbroeck.

Broos, ambaye amefundisha karibu nchi kibao za Ulaya, ni chaguo la kushangaza.
Hakuwemo katika orodha ya Fecafoot ya makocha watano, wakiwemo watatu Wafaransa, Mserbia na Mcameroon mmoja.

Broos ana uzoefu mkubwa kama kocha, alishinda ubingwa wa Ublgiji mara mbili akiwa na klabu ya Brugge na baadae akiwa na Anderlecht. Pia alifurahi kucheza katika timu ya Ugiriki, Uturuki katika miaka ya hivi karibuni.

Kibarua chake cha kwanza na timu hiyo ya Cameroon ni kutaka kuiweka timu hiyo kleleni katika mechi za kufuzu za Mataifa ya Afrika 2017 Kundi M, wakati itakapocheza na mchezo wa kufuzu nyumbani na ugenini dhidi ya Afrika Kusini mwezi ujao.

Pia kocha huyo atakuwa kibaruani wakati Simba hao wasiofungika watakapocheza na Ufaransa katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki mwezi Mei.

Van Gaal apokea kichapo England sasa akimbilia Ligi ya Ulaya




LONDON, England
LOUIS van Gaal alikiri kuwa kufuzu kucheza kwa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya itakuwa “ngumu sana” baada ya jana kupokea kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Sunderland iliyopo katika nafasi ya pili kutoka mkiani na kuongeza presha kwa kocha Manchester United.

Bao la kujifunga la dakika za mwisho kutoka kwa kipa David de Gea katika mchezo uliofanytika kwenye Uwanja wa Mwangaza kuliifanya Man United kufungwa kwa mara ya kwanza na Wearside katika kipindi cha miaka 19.

Kipigo hicho kimewaacha mabingwa hao mara 20 wa Ligi Kuu ya England kuwa pointi sita nyuma ya timu zinazoshika nafasi nne za kwanza zikiwa zimebaki mechi 12 kabla ya liugi kumalizika baada ya nahodha Wayne Rooney kuwa  "hayakuwa matokeo mazuri kabisa ".

Bao la 10 katika msimu la Anthony Martial kuliifanya Man United kusawazisha kabla ya mapumziko, likifuta lile la kuongoza la wapinzani wao lililowekwa kimiani na Wahbi Khazri, lakini Sunderland iliibuka na ushindi katika mchezo huo.

Ushindi huo umezidi kumuweka matatani Van Gaal, huku tetesi zikizagaa kuwa kocha wazamani wa Chelsea Chelsea Jose Mourinho anajiandaa kuchukua mikoba ya Mholanzi huyo mwishoni mwa msimu.

Van Gaal alisema kuwa kumaliza nafasi yanne ni “mahitaji madogo” kwao kwa klabu hiyo ya Man United.

"Ikiwa Wayne alisema itakuwa vigumu kwetu kumaliza katika nafasi nne za juu, baadae nakubalina naye. Itakuwa vigumu sana kutokana na nafasi yenyewe. Bado inawezekana lakini ni ngumu kweli.

"Tulitakiwa kushinda mchezo huu. Tunataka kuwa katika nafasi nne za mwanzo na sasa ni vigumu sana kuwa katika nafasi hiyo. Lakini hilo ndilo lengo letu, hiyo ni nafasi ya chini tunayohitaji kwa klabu kama hii. Huwezi kulifumbia macho hilo.”

United inaweza pia kufuzu kwa Ligi Kuu kwa kushinda Ligi ya Ulaya.
Timu hiyo itaifuata timu ya Denmark ya FC Midtjylland katika hatua ya 32 ya mashindano hayo Alhamisi na Van Gaal aliongeza: "Unaweza kusema ndio. Hiyo ni njia nyingine ya kufuzu. Lakini kuna baadhi ya vikosi vizuri sana vimeachwa katika mashindano hayo.”
 
Ronaldo azidi kumbeba Zidane Real Madrid 
 
MADRID, Hispania
KOCHA wa Real Madrid Zinedine Zidane ameendelea kumsimu mshambuliaji wake Cristiano Ronaldo baada ya Mredno huyo kufunga mabao mawili wakati kikosi chake kikiibuka na ushndi wa mabao 4-2 katika mchezo wa La Liga dhidi ya Athletic Bilbao.

Mabao hayo mawili ya Ronaldo yamemfanya kufunga bao moja zaidi ya mfungaji anayeongoza katika La Liga Luis Suarez baada ya kufunga mabao 21 katika mechi 32 alizocheza katika mashindano yote msimu huu.

Hatahivyo, mchezaji huy bora mara tatu wa dunia bado amekosolewa kwa kushindwa kuonesha makali yake ya kufunga mabao katika mechi kubwa za Real Madrid ugeni msimu huu.

"Vyombo vya habari viko hapa kwa ajili ya kuangalia kama Ronaldo anacheza vizuri au vibaya, lakini leo ameonesha mchezo mzuri na uwezo wa kufunga, “alisema Zidane.

"Kwangu mimi Cristiano ni mtu muhimu sana katika nafasi ya wingi. Wakati alipobadilisha mchezo hasa anapokuwa akikabiliana na mchezaji mmoja mmoja.

"Nia ni kucheza na Cristiano zaidi katika ushambuliaji wa pembeni…”

Ushindi huo umemfanya Zidane kuwa na mwanzo mzuri kama kocha wa Real Madrid tangu kuchukua nafasi ya Rafael Benitez mwizi uliopita na kutoka sare katika mechi sita za mwanzo.

Hatahivyo, Mfaransa huyo anakabiliwa na mtihani mkubwa hadi sasa wakati Real Madrid itakaporejea katika michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya ugenini dhidi ya Roma Jumatano.

Zaza aizamisha Napoli wakati Juventus ikishika usukani  Italia

ROME, Italia

MCHEZAJI tegemeo la Italia kwa michuano ya fainali za Mataifa ya Ulaya, Euro 2016, Simone Zaza alifunga bao safi katika dakika za mwisho wakati mabingwa Juventus wakiwa pointi moja mbele kileleni mwa Serie A ilipoibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Napoli Jumamosi.

Napoli, hicho ni kipigo chake cha tatu katika kampeni zake za kuwani ubingwa, ilisafiri kaskazini kwa ajili ya michezo miwili dhidi ya mabingwa hao kwa mara ya kwanza tangu katika kampeni za mwaka 2009-2010.

Kwa ushindi huo, Juventus sasa inaongoza katika msimamo wa ligi pamoja na Napoli, ambayo ina saka taji la kwanza tangu mwaka 1990 wakati Diego Maradona alipoiwezesha klabu hiyo ya kusini kutwaa taji lake la pili, sasa ni ya pili na inatofauti ya pointi moja.

Kocha Napoli Sarri wote walikiri kuwa safu ya ulinzi ya Juve ndio ilikuwa chanzo cha wao kufungwa: "Tulikuwa na bahati katika mita 20 mwisho.”

"Miezi nane iliyopita walikuwa pointi 24 nyuma yetu, sasa kama tumelingana.”

Chelsea yaikung'uta Newcastle mabao 5-1




LONDON, England
KLABU ya Chelsea jana ilipata ushindi wa kwanza wa nyumbani wa  Ligi Kuu ya England chini ya kocha wa muda, Guus Hiddink kwa ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya timu inayochechemea ya Newcastle.
Kikosi cha Hiddink kilichezea nyumbani mechi zake zote nne kwenye Uwanja wa Stamford Bridge tangu Mholanzi huyo achukue nafasi kutoka kwa mwenzake aliyetimuliwa Jose Mourinho kama kocha wa muda tangu Desemba.
Lakini Diego Costa ndiye aliyekuwa wa kwanza kuifungia Chelsea kwa bao la mapema kabla Pedro hajaongeza huku Willian na Bertrand Traore wakifunga na kuiwezesha timu hiyo kubuka na ushindi.
Mkosi katika mchezo huo uliibukia baada ya nahodha wa Blues John Terry kutoka nje ya uwanja baada ya dakika 37 kufuatia kuumia, kutokana na kugongana na Aleksandar Mitrovic.
Terry huenda asicheze mchezo wa Jumanne wa hatua ya 16 bora wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya dhidi ya Paris Saint Germain (PSG).
Ushindi huo ni maandalizi mazuri ya Chelsea kwa mchezo huo muhimu dhidi ya PSG, ambapo Pedro alionesha mchezoi mzuri.
Kikosi cha kocha Steve McClaren kilionekana kuwa katika hatari ya kushuka daraja baada ya kuporomoka tena hadi katika nafasi ya tatu mkiani chini ya Norwich kwa tofauti ya mabao.