Tuesday 31 March 2015

Real Madrid yasajili beki kisiki wa Porto



MADRID, Hispani
KLABU ya Real Madrid imethibitisha kumsajili beki wa kulia wa timu ya Porto ya Ureno Danilo (pichani) kwa ada ya uhamisho ya pauni Milioni 22.8, `aliyejifunga kuichezea timu hiyo hadi mwaka 2021.

Mbrazil huyo mwenye umri wa miaka 23, alikuwa akihusishwa na mabingwa hao wa Ulaya kwa miezi kadhaa huku Danilo wiki moja iliyopita alisikika akisema kuwa, anajivunia kuhusishwa na vijana hao wa kocha Carlo Ancelotti.

Na, Jumatano usiku, klabu hizo mbili zilitangaza kuwa beki huyo ataondoka Dragao katika kipindi cha majira ya joto na kusaini mkataba wa miaka sita huko Santiago Bernabeu.

"Porto walisema kuwa wamefikia makubaliano na Real Madrid kwa uhamisho wa kudumu wa Danilo kwa uhamisho wenye thamani ya euro Milioni 31.5," ilisema klabu hiyo ya Ureno.

Real Madrid ilithibitisha katika taarifa yake kuwa Danilo atajiunga na vigogo vya soka vya Hispania.

No comments:

Post a Comment