MONACO, Ufaransa
BEKI wazamani wa Chelsea amesema kuwa ushindi wa 3-1 wa
timu yake katika mchezo wa kwanza sio wakushangaza, lakini anakiri kuwa Monaco
bado haijajihakikishia nafasi ya kutinga robo fainali.
Beki wa Monaco Ricardo Carvalho alisema ushindi wao huo
wa 3-1 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya dhidi ya Arsenal hauipi
nafasi ama Arsene Wenger au timu yake.
Kabla ya kucheza mchezo wa marudiano Jumanne, Carvalho – ambaye
alikuwa ameumia katika mchezo wa kwanza, alisema kuteleza kwa Arsenal ni sehemu
ya mchezo, na Monaco nao wanaweza kupoteza faida ya kucheza nyumbani katika
mchezo huo wa Jumanne.
"Sijui [kama Arsenal wanaidharau Monaco]. Sifikirii
hivyo," alisema beki huyo wa kati wazamani wa Chelsea. “Wakati fulani hilo hutokea
katika soka. Ni kweli, kwa wengi ni jambo la ajabu.
"Arsenal ni timu kubwa, lakini wakati fulani
katika soka, ni kweli hilo linaweza kutokea. Hivyo inaweza kutokea tukiwa kwetu
nyumbani, kwa sababu katika soka huwa kuna aina kama ya maajabu kama hiyo.”
No comments:
Post a Comment