BAMAKO, Mali
MALI imeachana na
kocha Henryk Kasperczak (pichani) kufuatia timu hiyo kufanya vibaya katika fainali za
Kombe la Mataifa ya Afrika.
Shirikisho la Soka la Mali lilisema kuwa, baada ya kikao na kocha huyo mwenye umri wa miaka 68 raia
wa Poland "imekubaliwa kuwa tusiongeze mkataba wake".
Kasperczak alishindwa
kuivusha timu kutoka katika makundi katika mashindano ya hivi karibuni
yaliyomalizika Guinea ya Ikweta.
Mali ilimaliza na Guinea
lakini ilitolewa baada ya kutofanya vizuri.
Timu hiyo ilipanga
kumtangaza kocha mpya Machi 25 huku makocha wazamani Alain Giresse, Stephen
Keshi na Patrice Carteron wakiaminika kuwa majina yao yako mbele kujaza nafasi
hiyo.
No comments:
Post a Comment