LUMBUMBASHI, DR
Kongo
KIPA wa Ivory
Coast na TP Mazembe Sylvain Gbohouo (pichani)amekwenda Qatar kwa ajili ya matibabu ya
maumivu ya goti lake, imeelezwa.
Gbohouo alikuwa
kipa namba moja wa timu ya taifa ya Ivory Coast inayojulikana kama `Tembo’
katika fainali za Mataifa ya Afrika zilizofanyika Januari huko Guinea ya
Ikweta, ambako timu yao ilitwaa ubingwa.
Kipa huyo alikosa
fainali ya mashindano hayo dhidi ya Ghana baada ya kuumia goti lake wakati wa
mchezo wa nusu fainali dhidi ya DR Kongo.
Gbohouo bado
haijaichezea Mazembe ambao ni mabingwa mara nne wa Afrika, tangu aliporejea
kutoka katika fainali hizo za Mataifa ya Afrika.
Rais wa Mazembe Moise
Katumbi alisema kuwa Gbohouo aliruhusiwa kwenda kufanyiwa upasuaji kwa gharama
za Shirikisho la Soka la Ivory Coast.
"Aliondoka
wiki iliyopita na bado hajarudi, " alithibitisha Katumbi.
"Sio tatizo
kubwa sana lakini ni kwa ajili ya kutatua tatizo mara moja.
"Atarejea
katika mazoezi ya kawaida wiki tatu kuanzia sasa."
Katumbi, ambaye
kikosi chake wiki hii kitacheza na timu ya Afrika Kusini ya Mamelodi katika
raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika, alisema Mazembe itamtegemea
kipa mkongwe Robert Kidiaba wakati Gbohouo akiendelea kupona.
No comments:
Post a Comment