Tuesday 17 March 2015

Bondia Cheka sasa afungwa kifungo cha nje



Na Seba Nyanga, Morogoro
BONDIA wa ngumi za kulipwa Francis Cheka aliyekuwa akitumikia kifungo cha miaka mitatu gerezani amepunguziwa adhabu na sasa atatumikia kifungo cha nje, imeelezwa.

Cheka alipewa kifungo hicho na Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro baada ya kumtwanga meneja wake wa baa Bahati Kibanda hivi karibuni.

Cheka kuanzia jana alitakiwa kuanza kutumikia kifungo hicho cha nje baada ya maofisa huduma kwa jamii kutoka
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia na kufuata taratibu kwa makosa aliyotenda ili kuhakikisha anatumikia adhabu mbadala kwa jamii aliyoikosea.

Bondia Cheka alionekana mwenye uso wa furaha akiwa ndani ya viwanja vya mahakama, ambapo nje walikuwepo ndugu na jamaa zake, akiwemo mwalimu wake wa masumbwi, Salehe Abdallah au Komando.

Mbali na hao pia alikuwepo mdogo wake ambaye naye ni bondia, Cosmas Cheka ambao walikuwa wakimsubiri amalize taratibu na kutoka nje.
Bondia Francis Cheka.
Ofisa wa huduma kwa jamii mkoani Morogoro, Yusuph Ponela
alisema hayo jana mjini hapa mara bondia Cheka alipoletwa na maofisa wa Magereza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Mkoa kwa ajili ya kukamilisha taratibu kabla ya kuanza kutumikia kifungo hicho cha nje.

No comments:

Post a Comment