Monday 30 March 2015

Real Madrid wataka kumsajili Gareth Bale kwa pauni Mil.75



LONDON, England
KLABU ya Chelsea imeripotiwa inajiandaa kuilipa Real Madrid kiasi cha pauni Milioni 75 ili kumnasa Gareth Bale (pichani) kwa ajili ya kumsajili mchezaji huyo katika kipindi cha majira haya ya joto.

The Blues imekuwa ikihusishwa kwa kiasi kikubwa na Bale katika wiki chache zilizopita, huku ikidaiwa kukiwa na mazungumzo ya kujitoa Madrid.

Na sasa taarifa zinasema kuwa Chelsea wako tayari kulipa pauni Milioni 75 ili kumnasa mchezaji huyo.

Bale bado anangangania kuwa ana furaha Madrid na anatarajia kuendelea kuichezea timu hiyo, lakini Chelsea ilidokeza kutoa ofa ya pauni 300,000 kwa wiki kwa mchezaji huyo.

Huyo atakuwa mchezaji anayelipwa zaidi Chelsea kuwahi kutokea na hilo halitakuwa tatizo kwa klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment