Sunday 15 March 2015

Mourinho: Arsenal sasa imerejea katika mbio za ubingwa England




Nemanja Matic wa Chelsea akimuangusha chini Saido Mane na kuipatia Southampton penati iliyosawazisha bao na kuzifanya timu hizo kutoka sare 1-1.
LONDON, England
KOCHA wa Chelsea Jose Mourinho anadai kuwa Arsenal imerejea katika mbio za kuwania taji la Ligi Kuu ya England baada ya Chelsea kukaliwa kooni na kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Southampton.

Arsenal iliibuka na ushindi mnono wa bao 3-0 dhidi ya West Ham Jumamosi na kikosi hicho cha kocha Arsene Wenger, ambacho hakijashinda taji hilo tangu mwaka 2004, sasa kiko nyuma ya Chelsea kwa pointi saba tu.

Mabingwa wa England Manchester City wenyewe walijikuta wakipunguzwa kasi ya kutetea taji hilo baada ya kupokea kichapo cha bao 1-0 na Burnley huku Chelsea ikitoka sare kwenye uwanja wake wa Stamford Bridge.

Mourinho alisema: Bila shaka Arsenal wako katika mbio hizo. Wako pointi saba nyuma ya Chelsea, lakini ina mechi moja pungufu ya kucheza.

Timu zote City na Arsenal wako katika mbio za kuwania ubingwa. Itategemea hali ya Arsenal kwa sasa-kipigo cha bao 3-1 kutoka kwa Monaco au kipigo cha 3-0 dhidi ya West Ham?

Mourinho anaamini kuwa penati ya jana ilitolewa kimakosa na kuinyima kuwa point inane mbele ya Manchester City kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England.

Kocha huyo Mreno alipigwa faini ya pauni Milioni 25,000 kwa kitendo chake cha kusema kuwa 'kuna kampeni ya wazi'dhidi ya timu yake baada ya Cesc Fabregas kunyimwa penati na badala yake kupewa kadi kwa madai ya kujirusha katika sareya Desemba 28 kwenye uwanja wa St Mary's.

No comments:

Post a Comment