Monday 30 March 2015

Venus mbioni kukutana na dada yake Miami Open



MIAMI, Marekani
VENUS Williams (pichani)bado yuko katika mwelekeo wa kukutana na dada yake Serena katika fainali ya mashindano ya Miami Open baada ya kumtoa bingwa namba tano wa dunia Caroline Wozniacki katika hatua ya 16 bora.

Mmarekani huyo alimshindi mpinzani wake wa Denmark kwa 6-3 7-6 (7-1) ndani ya dakika 98.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34, ambaye kwa miezi saba alikuwa nje ya mchezo huo kutokana na maumivu mwaka 2011, sasa ameshinda mechi saba kati ya nane zilizopita dhidi ya wachezaji 10 bora.

Dada yake Serena alimchakaza Svetlana Kuznetsova 6-2 6-3 na kutinga robo fainali.

Mdada huyo mwenye umri wa miaka 33 atakutana na Sabine Lisicki katika robo fainali baada ya Mjerumani kumfunga Sara Errani 6-1 6-2.

Wakati huohuo, Venus, atakutana na Mhispania Carla Suarez Navarro, ambaye anarudi mchezoni baada ya kufungwa katika seti ya kwanza dhidi ya nMpoland anayeshika nafasi ya saba Agnieszka Radwanska 5-7 6-0 6-4.

Novak Djokovic, ambaye ndiye bingwa mtetezi kwa upande wa wanaume, alimsambaratisha Mbelgiji Steve Darcis 6-0 7-5.

No comments:

Post a Comment