Sunday 8 March 2015

Barcelona yashinda 6-1 na kuichomoa Real Madrid kileleni




Lionel Messi (kulia) akipongezana na Luis Suerez.
BARCELONA, Hispania
NYOTA Lionel Messi amefunga hat-trick yake ya 24 katika Ligi Kuu ya Hispania ya La Liga wakati Barcelona ikitinga kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo.

Barca ilitumia vizuri nafasi ya Real Madrid kufungwa na Athletic Bilbao wakati Luis Suarez pia akizifumania nyavu mara mbili wakati timu hiyo ikiibuka na ushindi wa bao 6-1 dhidi ya Rayo Vallecano.

Suarez aliifungia timu yake bao la kuongoza na Gerard Pique akipachika la pili kabla ya Messi hajafunga la tatu katika dakika ya 12 ya mchezo huo.

Mara mbili alifunga kwa penati, ambapo alifunga la nne kabla hajapachika la tano na Suarez alifunga tena.

Timu zote mbili zilijikuta zikimaliza mchezo zikiwa na wachezaji 10 wakati Román Triguero alipooneshwa kadi ya pili ya njano kwa kumuangusha Suarez, na kusababisha penati iliyomuwezesha Messi kufanya matokeo kuwa 3-0.

Barca nao walijikuta wakipata pigo baada ya beki wao Dani Alves kutolewa nje baada ya kumchezea vibaya Bueno wakati akielekea langoni na Rayo alifunga penati hiyo na kumfanya kuwa na mabo 13 katika La Liga.

Messi sasa ana mabao 30 ya ligi, ikiwa ni sawa na mshabuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo, ambaye hat-trick zake 23 katika La Liga zimezidiwa na Messi mara moja.

Mess ambaye ni mchezaji wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 27 , sasa anashikilia rekodi ya kuwa mchezaji aliyefunga hat-trick nyingi zaidi katika soka la Hispania.

No comments:

Post a Comment