Saturday 21 March 2015

Kluivert:Messi, Ronaldo wananogesha ushindani Hispania



MADRID, Hispania
NYOTA wazamani wa Barcelona anaamini kuwa endapo mmoja kati ya nyota hawa wawili wa La Liga ataondoka katika klabu yake ya sasa, hakuna shaka kuwa itapungusa sana ushindani wao.

Mshambuliaji wazamani wa Barcelona Patrick Kluivert (pichani), anaamini kuwa ni muhimu kwa Lionel Messi na Cristiano Ronaldo kuendelea kubaki Hispania ili kuweka hai upinzani wao.

Wawili hao wanacheza timu tofauti za Barca na Real Madrid zinazoshiriki Ligi Kuu ya Hispania ya La Liga tangu Ronaldo ajiunge mwaka 2009, huku Messi akiwa Camp Nou tangu mchezaji huyo aanze kuichezea kwa mara ya kwanza timu hiyo miaka mitano kabla.

Wawili hao ndio wamekuwa wakitaweala tuzo za mchezaji bora wa dunia au Ballon d'Or kwa miaka saba mfululizo, huku Messi akishinda tuzo hizo mara nne na Mreno Ronaldo akitwaa mara tatu, huku viwango vyao vya ajabu vikileta malumbano miongoni mwa wapenda soka.

 Kluivert,aliyeichezea Barcelona kwa miaka saba kuanzia mwaka 1998, anafikiri arjen Robben wa Bayern Munich ndiye mchezaji pekee anayewakaribia wachezaji hao wawili kwa viwango kwa sasa.

"Wote ni wachezaji wazuri ," alisema kocha huyo wa Curacao katika mtandao wa Shirikisho la Kimataifa la Soka (Fifa). "Kitu muhimu sana ni kuwa wote kwa sasa wanacheza soka Hispania. Endapo mmoja angekuwa Hispania na mwingine England, upinzani ungekuwa tofauti.

"Lakini, acha tuseme ukweli, wachezaji wote ni bora duniani na baadae ndio anakuja Robben na wengine. Messi ni mchezaji wa aina yake: mguu wake wa kushoto ni kama dhahabu. Kila anachofanya kinafanana na dhahabu.

No comments:

Post a Comment