Saturday 30 September 2017

Msomi Chuo Kikuu kuongoza Chaneta, Judith Ilunda amuangusha Mama Mbiro katika Ukatibu Mkuu

Na Mwandishi Wetu
MKUFUNZI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Idara ya Physical Education and Sports Scince, Dk Devotha Marwa ndio mwenyekiti mpya wa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta) baada ya kumshinda Damian Chonya katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika leo mjini Dodoma.

Ofisa Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Halima Bushiri anasema kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chaneta sasa ni Anna Gidalia wakati Katibu Mkuu ni mchezaji wazamani wa timu ya taifa ya netiboli ya Tanzania, Judith Ilunda huku msaidizi wake ni Hilda Mwakatobe.

Ilunda alimshinda makamu mwenyekiti aliyemaliza muda wake katika Chaneta, Zainabu Mbiro ambaye aliamua kuwania ukatibu mkuu badala ya umakamu wa rais.

Nafasi ya Uhazini imebaki wazi baada ya mgombea pekee Grace Khatibu kuata kura chache sana na kuamuriwa uongozi mpya wa Chaneta kuandaa uchaguzi mdogo kwa ajili ya kuziba nafasi hiyo ya uhazini.

Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ni pamoja na Yasinta, Julieth, Kilongozi, Asha, Fortunata na Lwiza.

Uchaguzi huo ulisimamiwa na BMT, ambao waliendesha mchujo jana Ijumaa na kumchuja aliyekuwa mwenyekiti wa Chanea, Annie Kibira na kumtaka kuwa mshauri kutokana na hali yake ya afya kutokuwa nzuri.

Maghembe, Msigwa watembelea banda la TAA Maonesho ya Utalii Karibu Kusini 2017 Iringa

Waziri wa Maliasili na Utalii,  Prof. Jumanne Maghembe (kushoto),aliyefungua rasmi maonesho ya Utalii ya Karibu Kusini,  akikaribishwa na Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Iringa,  Hana Kibopile  kwenye banda la maonesho la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), yanayofanyika kwenye viwanja vya Kichangani..
Mhandisi Kedrick Chawe (kulia) akisalimiana na mgeni rasmi wa maonesho ya Utalii ya Karibu Kusini, Waziri wa Maliasili na utalii, Mhe. Prof. Jumanne Maghembe. Wengine katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza (mwenye ushungi mweupe) na wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Bw. Richard Kasesela.



 Mbunge wa Iringa, Mchungaji Peter Msigwa (kushoto) akizungumza na  Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Iringa  Hana Kibopile alipotembelea banda la maonesho ya Utalii ya Karibu Kusini  la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA).
Ofisa Usalama wa Kiwanja cha ndege cha Iringa kilichopo Kata ya Nduli, Miyaga Watanda (kulia) akitoa maelezo mbalimbali kwa wanafunzi wa shule ya Wasichana ya Iringa walipotembelea banda la maoneksho ya Utalii ya Karibu Kusini la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA).   

Friday 29 September 2017

Cecafa yaipa Kenya uenyeji Kombe la Chalenji 2017

NAIROBI, Kenya

BARAZA la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki (Cecafa) limeitangaza Kenya kuwa mwenyeji wa mashindano ya Chalenji ya wakubwa, ambayo hayajafanyika kwa miaka miwili sasa.

Kwa mara ya mwisho mashindano hayo ya Chalenji yalifantyika Ethiopia na Uganda ndio ilitwaa ubingwa huo.

Katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya Cecafa kilichodanyika Khartoum, Sudan, wajumbe walionesha msiokamano na Kenya dhidi ya kupokonywa uenyeji wa mashindano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani, Chan Januari 2018.

 

Mashindano  ya wakubwa ya Chalenji yanashirikisha mataifa yote 13 wanachama wan chi za Afrika Mashariki na Kati, yatafanyika Novemba na Desemba mwaka huu.

Uganda ndio mabingwa wasasa wa mashindano hayo baada ya kutwaa kwa ara ya mwisho mwaka 2015 baada ya kuifunga Rwanda 1-0 katika fainali.

Mkutano huo pia ulizitangaa Burundi na Rwanda kuwa wenyeji wa mashindano ya Cecafa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 na yale ya wanawake Novemba na Desemba.

 

Thursday 28 September 2017

Maghembe Kufungua Maonesho ya Utalii Karibu Kusini yanayofanyika Kihesa mkoani Iringa

Mhandisi Kerdick Chawe (kushoto) akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza (mwenye ushungi) kwenye banda la maonesho la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), wanaoshiriki kwenye maonesho ya Utalii ya Karibu Kusini yanayofanyika kwenye viwanja vya Kichangani mkoani Iringa.

Na Mwandishi Wetu,Iringa

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe leo Ijumaa  atafungua rasmi maonesho ya Utalii ya Karibu Kusini kwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim, yanayofanyika kwenye viwanja vya Kichangani mkoani Iringa.

Maonesho hayo yenye kaulimbiu ya Utalii Endelevu ni Nguzo ya Uchumi wa Viwanda yanashirika taasisi za serikali, mashirika ya umma na kimataifa zaidi ya 400, ambapo yatamalizika Oktoba 2, 2017, ambapo yanalengo la kuweka uelewa kwa jamii kuhusu umuhimu wa utalii na thamani thamani ikiwa ni pamoja na kuutangaza utalii kwa kuihamasisha jamii kutumia fursa za utalii zilizopo katika kuinua uchumi wa wakazi wa Ukanda wa Kusini mwa Tanzania na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wa Wizara mbalimbali zipo na taasisi zake ikiwemo Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Idara ya Utalii, Wanyamapori, Mambo ya Kale na Misitu na Nyuki, Chuo cha Taifa cha Utalii, Makumbusho ya Taifa, Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Mamlaka ya Usimamizi ya Wanyamapori (TAWA) Mfuko wa Misitu Tanzania  (TaFF).

Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Bw. Richard Kasesela  (kulia) akisalimiana na Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Iringa kilichopo Kata ya Nduli, katika banda la maonesho ya Utalii ya Karibu Kusini la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), yanayofanyika kwenye viwanja vya Kichangani mkoani Iringa.

Taasisi nyingine ni Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, (TFS)  Taasisi ya Utafiti wa Misitu na Wadau wa Wizara ya Maliasili na Utalii.Wadau wa Sekta ya Utalii kutoka mikoa  ya Nyanda za Juu Kusini watashiriki kuonesha bidhaa na huduma zao muhimu na mikoa inayoshiriki ni pamoja na wenyeji Iringa, Mbeya, Ruvuma, Songwe na Njombe.

Ofisa Uhusiano wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bi. Bahati Mollel akimkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Bw. Richard Kasesera katika banda lao la maonesho ya Utalii ya Karibu Kusini yanayofanyika kwenye viwanja vya Kichangani mkoani Iringa.

Fursa zilizopo nyanda za Juu Kusini ni pamoja na Ziwa Tanganyika, Ziwa Rukwa,  Ismila,Kalenga na Boma la Mkuu wa Wilaya, Hifadhi za Mahale, Katavi, Ruaha, Kitulo na Selous.




Monday 25 September 2017

LONDON, England

TIMU ya Brighton imeichapa Newcastle United bao 1-0 na kupata ushindi wa pili mfululizo katika mechi za Ligi Kuu ya England.

Wenyeji walipata bao wakati krosi ya Pascal Gross iliporejeshwa nyuma kwa kichwa na Dale Stephens na Tomer Hemed alifunga kutoka umbali wa meta sita.

Newcastle, ambayo ilishinda mechi zake tatu zilizopita, ilikuwa na nafasi, lakini mpira wa Mikel Merino ulipanguliwa na Mat Ryan, huku Joselu mara mbili akishindwa kufunga na mchezaji aliyetokea benchi Jonjo Shelvey, shuti lake likigonga mwamba.

Ushindi huo umeiwezesha Seagulls kupaa hadi nafasi ya 13 katika msimamo, wakati Newcastle imeporomoka hadi nafasi ya tisa.

Newcastle ilitawala zaidi mchezo huo na kupiga mashuti mengi lakini kikosi hicho kinachofundishwa na Rafael Benitez, kilishindwa kulazimisha sare.

Wachezaji waliongia wakitokea benchi Jesus Gamez na Dwight Gayle jitihada zao za dakika za mwisho zilishindwa kuzaa matunda, ambapo mashuti yao yaliokolewa na Ryan.

Wagombea Chaneta kupiga kampeni kiduchu

Annie Kibira

Na Mwandishi Wetu

WAGOMBEA watakaopitishwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika Uchaguzi Mkuu wa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta) Jumamosi mjini Dodoma, watakuwa na muda mfupi wa kujinadi.

Kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi huo iliyotolewa na Baraza la Michezo la Taifa (BMT), mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni Alhamisi wakati usaili utafanyika Ijumaa na uchaguzi Jumamosi.

Mwenyekiti wa Chaneta, Annie Kibira amesema leo kuwa muda wa kampeni ni mdogo sana, lakini itabidi kufuata utaratibu uliowekwa na BMT, ambao ndio wasimamizi wa uchaguzi huo.

Alisema hawaruhusiwi kufanya kampeni hadi baada ya usaili kwani kutofuata utaratibu huo, unaweza kukatwa kwani utakuwa umekiuka utaratibu.

Halima Bushiri;Ofisa Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT).

Naye Ofisa Michezo wa BMT, Halima Bushiriki amesema leo kuwa wamepanga ratiba hiyo ili kuwaepuesha wagombea na wapiga kura kuingia gharama.

Alisema hadi jana wagombea 14 wanaotaka kugombea nafasi mbalimbali walirudisha fomu kati ya 25 waliochukua fomu hizo, huku akiwasisitizia watu kuendelea kuchukua na kurudisha kwa wakati ili kufanikisha zoezi hilo.

Pia aliwataka wadau mbalimbali wa michezo bila kujali jinsi, yaani wanawake na wanaume wenye sifa  kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu hizo ili kugombea uongozi.

Aliwataja waliorudisha hadi jana kuwa ni Annie Kibira (uenyekiti), Dk Devota Muro, Luiza Jellah (ujumbe), Mwajuma Kisengo (katibu msaidizi/mjumbe), Asha Sapi (ujumbe) na Winfrida Emmanuel (makamu mwenyekiti),

Wengine waliorejesha fomu ni Hilda Mwakatobe (katibu msaidizi), Judith Ilunda (katibu mkuu/ujumbe), Zakia Kondo (ujumbe), Julieth Mndeme (ujumbe), Pili Mongella (makamu mwenyekiti/ujumbe).

Kocha Mourinho anusurika na adhabu zaidi

LONDON, England

KOCHA wa Manchester United, Jose Mourinho (pichani) hataadhibiwa zaidi baada ya Jumamosi kutolewa uwanjani wakati timu yake ikicheza dhidi ya Southampton.

Mourinho alitolewa nje na mwamuzi Craig Pawson baada ya kuingia uwanjani katika dakika za majeruhi katika mchezo ambao timu yake ilishinda bao 1-0 kwenye Uwanja wa St Mary's.

Baada ya kupokea taarifa ya mwamuzi, Chama cha Soka (FA) kiliamua kutomuongezea adhabu kocha huyo.


Mourinho alifungiwa kuhudhuria mechi mbili na FA msimu uliopita kutokana na matukio tofauti.

Valencia yaipiku Real Madrid katika La Liga

MADRID,Hispania

VALENCIA imewapiku mabingwa watetezi wa La Liga Real Madrid kwa kupanda hadi nafasi ya nne wakati bao la ushindi likifungwa na Simone Zaza dakika tano kabla ya mchezo kumalizika na kushinda 3-2 dhidi ya Real Sociedad jana.

Hatahivyo, kocha wa Valencia Marcelino alijikuta matatan baada ya kujmia misuli wakati akishangilia ushindi wa timu yake.

Marcelino aliumia misuli katika mguu wake wa kushoto wakati akishangilia goli la ushindi la Simone Zaza alilofunga katika dakika ya 85 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Anoeta.

"Nimezeeka, nahitaji kujizuia katika hali fulani, “alisema kocha huyo mwenye umri wa miaka 52 huku akitabasamu. "Wakati kocha anapoumia, hilo sio tatizo.”

Valencia ilishinda mabao 3-2 na kuendeleza rekodi ya kutofungwa na kupaa hadi katika nafasi ya nne katika msimamo wa La Liga wakati Real Madrid wako katika nafasi ya tano.


Jumla ya mabao 20 yalifungwa katika mechi za La Liga Jumapili wakati Espanyol, Getafe na Celta Vigo nazo pia ziliposhangilia ushindi.

Mashabiki wa soka wafungwa maisha Misri

CAIRO, Misri

MAHAKAMA ya Misri imewahukumu vifungo vya maisha watu wawili kutokana na vurugu zilizosababisha vifo vya watu kibao kwenye Uwanja wa soka mjini hapa Februari 2015.

Angalau watu 19 walikufa uwanjani baada ya polisi kulipua gesi ya kutoa machozi kwa mashabiki wakati wakijaribu kulazimisha kuingia kwenye Uwanja wa Jeshi la Anga.

Watuhumiwa wengine 12 walifungwa vifungo vya kati ya miaka miwili hadi 10 kwa kuhusu kwao katika dhahama hiyo, ambapo wengine wawili waliachia huru.

Tukio hilo lilitokea kabla ya mchezo kati ya Zamalek na  Enppi.

Mchezo huo ulikuwa wa kwanza wa ligi kubwa nchini Misri kuruhusiwa mashabiki kuingia uwanjani baada ya mashabiki kuzuiwa kushuhudia mechi kutokana na watu zaidi ya 70 kufa uwanjani huko Port Said mwaka 2012.

Watuhumiwa hao walikuwa wakikabiliwa na makosa ya mauaji, kuleta vurugu, na walikuwa wakishtakiwa kukombana na polisi, na kusababisha vurugu.

Pamoja na wawili kufungwa maisha, watatu walifungwa miaka 10, watano wamefungwa miaka saba, watatu walifugwa jela miaka mitatu kila mmoja na mmoja alifungwa miaka miwili.

Washtakiwa wote walikuwpo mahakamani wakati wa hukumu hiyo na ruksa kukata rufaa.


 

Brighton yaichapa Newcastle United bao 1-0

Mshambuliaji wa Brighton, Tomer Hemed (kushoto) akiwania mpira na beki wa Newcastle United, DeAndre Yedlin wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya England uliofanyika kwenye Uwanja wa American Express Community huko Brighton, kusini mwa England jana. Brighton ilishinda 1-0. 

LONDON, England

TIMU ya Brighton imeichapa Newcastle United bao 1-0 na kupata ushindi wa pili mfululizo katika mechi za Ligi Kuu ya England.

Wenyeji walipata bao wakati krosi ya Pascal Gross iliporejeshwa nyuma kwa kichwa na Dale Stephens na Tomer Hemed alifunga kutoka umbali wa meta sita.

Newcastle, ambayo ilishinda mechi zake tatu zilizopita, ilikuwa na nafasi, lakini mpira wa Mikel Merino ulipanguliwa na Mat Ryan, huku Joselu mara mbili akishindwa kufunga na mchezaji aliyetokea benchi Jonjo Shelvey, shuti lake likigonga mwamba.

Ushindi huo umeiwezesha Seagulls kupaa hadi nafasi ya 13 katika msimamo, wakati Newcastle imeporomoka hadi nafasi ya tisa.

Newcastle ilitawala zaidi mchezo huo na kupiga mashuti mengi lakini kikosi hicho kinachofundishwa na Rafael Benitez, kilishindwa kulazimisha sare.


Wachezaji waliongia wakitokea benchi Jesus Gamez na Dwight Gayle jitihada zao za dakika za mwisho zilishindwa kuzaa matunda, ambapo mashuti yao yaliokolewa na Ryan.

Sunday 24 September 2017

Tigo Fiesta 2017 yafunika kinoma Mwanza

 Ben Pol akifanya vitu vyake kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Na Mwandishi Wetu, Mwanza

NAWEZA  kusema ilikuwa shoo ya aina yake ambayo mikoa mingine ilikopita Tigo Fiesta 2017 mwaka huu haijatokea. Watu waliitikia wito kwa kuujaza Uwanja wa CCM Kirumba na kupata walichotarajia.

Ufunguzi wa jukwaa uliofanya na msanii wa kufokafoka Rosa Ree, ambaye alionesha jinsi gani anakuja kwa kasi kubwa na nyimbo zake zikiwemo mchaga mchaga na up in the air na kufuatiwa na Lulu Diva

 Sehemu ya umati wa wapenzi wa muziki waliofunika CCM Kirumba, Mwanza.

Wasanii Rostam akiwemo Roma na Stamina wao walikuja kivingine walipopanda jukwaani kila moja na baiskeli yake na kuweka kitu tofauti kwenye wimbo wao huku ama kule, kwa kweli ilikuwa burudani tosha.

Wasanii wengine waliofanya shoo iwe na bora kuliko zilizopita ni Ommy Dimpoz na Rayvanny ambao hawakushiriki tamasha zilizopita kila mmoja kwa nafasi yake alikonga nyoyo za masha
biki.

Ali Kiba akifunika.

 Msanii ambaye alifunika wote ni Alli Kiba a.k.a King Kiba kwa kweli aliitendea haki steji mashabiki hawakutaka ashuke kila wakati wanaomba arudie kibao chake 'SEDUCE' huu ni wimbo mpya wa Kiba ambao umetokea kupendwa kila kona alirudia mara tatu kutokana na maombi ya mashabiki.

 Kwa upande wa wadhamini Tigo, Meneja wa Tigo Kanda ya Ziwa, Edgar Mapande alisema mwaka huu tumeamua kudhaminj ili kusaidia vipaji vya wasanii na kuwaletea wateja wetu burudani, kadhalika kuwapatia vifurishi mara wanunuapo tiketi za Tigo Fiesta . Mteja wetu akinunua tiketi anapata Mbs 100, dakika 100 na sms 100 bure .

Tamasha linaendelea ijumaa ijayo mkoani Tabora kwenye Uwanja wa Ali  Hassan Mwinyi.






Tuesday 19 September 2017

Tetemeko la Ardhi laua Watu 140 nchini Mexico

MEXICO CITY, Mexico

TETEMEKO kubwa la ardhi limeikumba Mexico na kupoteza maisha ya zaidi ya watu 140 na kuharibu majengo mengi katika jiji hili, imeelezwa.

Angalau watoto 21 wanahofiwa kufa na wengine wakiripotiwa kupotea baada ya shule kuanguka katika jiji hilo.

Tetemeko hilo linalokadiriwa kuwa na ukubwa wa magnitude 7.1 pia limesababisha uharibifu mkubwa katika nchi za jirani.

Kwa mara ya mwisho tetemeko kubwa kama hilo liliwahi kutokea takribani miaka 32 iliyopita baada ya tetemeko kuua maelfu ya watu Mexico City.

Hilo ni tetemeko la pili kutokea baada ya lile la mapema mwezi huu ambalo lilikuwa na ukubwa na magnitude 8.1 ambalo liliua watu 90 lilitokea kusini mwa nchi hii.

Angalau watu 149 wamekufa nchi nzima, kimeeleza chanzo kimoja cha habari.

Angalau watu 55 wamekufa katika Jimbo la Morelose,kusini mwa Mexico City, huku 32 wakifa huko Pueblae. Watu 49 wanahofiwa kupoteza maisha Mexico City, huku wengine 10 wakifa katika Jimbo la Mexico, na watau wakifa huko Guerrero.

Karibu watu milioni 2 wakazi wa Mexico City wameachwa bila ya umeme huku nyaya za simu zikiwa zimeanguka. Wananchi wameonywa kutovuta sigara mitaani kwani gesi inaweza kulipuka.

Meya wa Mexico City Miguel Angel Mancera aliaimbia TV moja kuwa huduma za uokoaji zinaendelea kuchimba katika makazi 44 ili kuona kama kuna watu wamefukiwa na kifusi.

Kaimu Katibu wa Elimu Javier Treviño, alikaririwa na vyombo vya habari vya haba kuwa, watoto 21 na watu wazima wanne walikufa wakati shule ya Enrique Rebsamen iliyopo kusini mwa Mexico City ilipoanguka.

Baadhi ya wanafunzi waliokolewa, vyombo vya habari vya Mexico viliripoti, lakini wengine bado hawajapatikana.

Nyumba za gholofa, maduka makubwa na kiwanda navyo pia ni baadhi ya vitu vilivyoanguka jijini hapa.

Akihutubia kupia televisheni, Rais wa Mexico Peña Nieto alisema dharura imechukulia katika maeneo yaliyoathirika na jeshi limekwenda kutoa msaada.

Karibu sehemu zote katika jiji la Mexico, timu ya watu wa uokoaji na wake wakujitolea wamekuwa wakifanya jitihada mbalimbali kuwaokoa watu.

"Mke wangu yuko pale. Sijaweza kuwasiliana naye, “alisema Juan Jesus Garcia, 33, huku akitokwa na machozi jirani na jengo lililoanguka.

"Hajaweza kujibu simu na sasa tumeambia kuzima simu zetu za viganjani kwa sababu kuna gesi inayovuja inaweza kulipuka.”

Tetemeko hilo la ardhi limetokea  jijini Mexico wakati wa kumbukumbu ya miaka 32 ya tetemeko jingine la ardhi lililoua watu 10,000.


Mexico City ni moja ya majiji yenye watu wengi duniani, ambapo ina zaidi ya wakazi milioni 20 wanaoshi hapo.

Messi atupia manne Barca ikishinda 6-1

BARCELONA, Hispania

LIONEL Messi ameongeza mabao manne katika akaunti yake aliyofunga mapema msimu huu wakati Barcelona ikiendeleza kwa asilimia 100 rekodi yake ya ushindi katika Ligi Kuu ya Hispania ya La Liga baada ya kuifunga Eibar 6-1 jana.

Paulinho na Denis Suarez nao pia walizifumania nyavu katia mchezo wa pili mfululizo wakati Barca ikizidi kujitanua kileleni katika ,simamo wa ligi hiyo hadi kufikia pointi saba zaidi dhidi ya wapinzani wao wakubwa, Real Madrid, ambayo leo watakuwa wenyeji wa Real Betis.

Mapema, Valencia ilipanda hadi katika nafasi ya tatu wakati Simone Zaza alipofunga mabao matatu `hat-tric’ ndani ya dakika saba wakati timu hiyo ikiisambaratisha Malaga kwa mabao 5-0.

Kocha wa Barca Ernesto Valverde alikibalisha sana kikosi chake kwa mara ya kwanza tanbgu alipoanza kuifundisha timu hiyo, ambapo alibadili wachezaji sita kutoka katika kikosi kilichocheza Jumamosi na kushinda 2-1 dhidi ya Getafe.


Messi alianza kufungua akaunti ya mabao katika mchezo huo baada ya kufunga kwa penalti katika dakika ya 21 baada ya Nelson Semedo kuchezewa vibaya  na Alejandro Galvez.

MSIMAMO LA LIGA:


PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Barcelona55001721515
2Sevilla431061510
3Valencia52309369
4Real Sociedad430111749
5Real Madrid42209458
6Atlético Madrid42208358
7Athletic Club42113127
8Villarreal42026516
9Levante41305416
10Leganés42023306
11Las Palmas420257-26
12Real Betis420257-26
13Eibar5203310-76
14Getafe411234-14
15Girona411235-24
16Espanyol411238-54
17Celta de Vigo410357-23
18Deportivo La Coruña4013511-61
19Deportivo Alavés400407-70
20Málaga5005111-100