Sunday 29 March 2015

Ujamaa Intellectuals Network watoa msaada kwa watoto yatima


Ubosi pembeni!:Mratibu wa taifa wa taasisi ya Ujamaa Intellectuals Network (UIN), Lusekelo Nelson Mwandemange akipeleka kiroba cha unga katika kituo cha watoto yatima cha Maunga kilichopo Kinondoni Hananasif Jumapili.

Na Mwandishi Wetu
TAASISI ya Ujamaa Intellectuals Network (UIN) Jumapili ilitoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha Maunga kilichopo Hananasif Kinondoni Moscow jijini Dar es Salaam.

Taasisi hiyo kupitia idara yake ya jamii, ilitoa vifaa hivyo vilivyokabidhiwa kwa kiongozi na mmiliki wa kituo hicho Bi.Zainab Bakari Maunga ni pamoja na unga, sabuni, madaftari, chumvi, juice, mafuta ya kula, mafuta ya kupaka na vitu vingine.

Mratibu taifa wa UIN Lusekelo Mwandemange ndiye aiyekuwa wa kwanza kukabidhi baadhi ya vifaa hiyo kwa Bi. Maunga kabla ya wana taasisi wengine nao kukabidhi baadhi ya vifaa hivyo.

Kituo hicho kina jumla ya watoto yatima 49 huku baadhi yao wakiwa ni wanafunzi wa chekechea, shule ya msingi na watatu wako sekondari.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo Bi. Maunga alishukuru sana kwa msaada huo na alitaka wasamaria wema wengine kujitokeza kuwasaidia kama walivyofanya UIN.

 Naye Mwandemange alisema mbali na msaada huo, UIN pia kina mpango wa kuwasaidia wanafunzi hao watatu wanaosoma sekondari.

Pia aliwataka watu na tasisi zingine kujitokeza kwa wingi kusaidia kituo hicho ili kuhakikisha watoto hao yatima nao wanapata elimu kama watoto wengine.
Mkamiti Mgawe akibeba ndoo ya mafuta ya kula katika kituo cha watoto yatima




   
 





 


No comments:

Post a Comment