KIGALI,Rwanda
RAIA wa Ireland ya
Kaskazini Johnny McKinstry (pichani) yuko mbioni kuifundisha timu ya taifa ya Rwanda
baada ya kuwamo katika orodha ya watu wanne wanaowania nafasi hiyo.
Wengine wanaowania
kibarua hicho ni pamoja na kocha msaidizi wazamani wa Chelsea Jose Morais, kocha
wa Uturiki Engin Fırat na Mjerumani Hans
Michael Weiss.
Rwanda inaangalia
mbadala wa kocha Muingereza Stephen Constantine, aliyejitoa tangu Januari na
kwenda kuwa kocha wa timu ya taifa ya India.
Kocha wazamani wa Sierra
Leone McKinstry, 29, inafikiriwa ndiye
anayepewa nafasi kubwa ya kunasa kibarua hicho.
Aliteuliwa kuwa
kocha wa Leone Stars akiwa na umri wa miaka 27 na kuiongoza timu hiyo hadi
kufikia nafasi ya 50 katika viwango vya ubora vya Shirikisho la Kimataifa la
Soka (FIFA), akipotezamchezo mmoja tukati ya sitaya kwanza.
Lakini kufuatia
kufungwa na Ivory Coast na Kongo ya DRC katika fainali za Mataifa ya Afrika,
alitimuliwa ikiwa ni miezi sita tu tangu alipopewa kazi hiyo kwa misingi ya
kudumu.
Kocha Mreno Morais,
49, alifanya kazi kama msaidizi wa Jose Mourinho katika timu ya Inter Milan, Real
Madrid na Chelsea kabla hajaenda timu ya Tunisia ya Esperance.
No comments:
Post a Comment