HARARE, Zimbabwe
ZIMBABWE imeondolewa katika kinyang’anyiro cha kufuzu kwa fainali za Kombe la dunia za mwaka 2018
baada ya nchi hiyo kushindwa kumlipa kocha wake wazamani Jose Claudinei
Georgini.
Shirikisho la Kimataifa la Soka (fifa) limesema katika taarifa
yake kuwa limechukua hatua hiyo “kama matokeo
ya kutolipa deni lake".
Fifa iliongeza kuwa Chama cha Soka cha Zimbabwe (zifa0 kilishindwa
kufanya malipo licha ya kupewa muda kufanya hivyo.
Hatua hiyo ya kuifungia Zimbabwe kumemaliza nafasi ya nchi hiyo kucheza
fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Russia mwaka 2018 hata kabla timu yao
ya taifa haijagusa mpira.
Kanda ya Afrika inatarajia kuanza harakati za kusaka tiketi ya
kucheza fainali hizo Oktoba, huku ratiba kamili inatarajia kupangwa huko St
Petersburg mwezi julai, Zimbabwe haijawahi kufuzu kucheza fainali za Kombe la
Dunia.
Mbrazil Georgini, aliyepewa jina la utani la Valinhos, na alianza
kuifundisha timu hiyo januari hadi Novemba mwaka 2008. Na alikuwa akiidai Zifa
na kwa mara ya kwanza Fifa ilikitaka chama hicho cha soka kumlipa kocha huyo
mwaka 2012.
Zimbabwe mara kadhaa ilipewa hatmatamu na onyo lakini ilipuuza
maagizo hayo ya Fifa. Fifa imesema kuwa Zimbabwe haikukata rufaa dhidi ya
adhabu hiyo.
Zifa inakabiliwa na ukata mkali wa fedha, ikiwa na madeni karibu
dola za Marekani Milioni 4, na hivi karibuni iliuzaa vifaa vyake vilivyomo
katika kituo cha mazoezi ilichojengewa na Fifa ili kupunguza ukata huo.
No comments:
Post a Comment