Sunday 28 July 2019

Askari, Mbwa Kuongezwa Viwanja vya Ndege

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni (kulia) akiongozana na maafisa wa ulinzi na usalama kukagua sehemu za kupitisha mizigo kwenye Jengo la tatu la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa la Julius Nyerere (JNIA TB3), alipofanya ziara hivi karibuni.

Na Mwandishi Wetu
Wizara ya Mambo ya Ndani nchini, itaongeza askari watu na mbwa kwa ajili ya kuimarisha ulinzi na usalama kwenye viwanja vya Ndege nchini.

Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Hamad Masauni amesema hayo alipofanya ziara ya kikazi katika Jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA TB3).

Masauni amesema serikali inatarajia kuongeza askari mbwa wengi wenye mafunzo na sifa, ili kuongeza ufanisi na ulinzi wa viwanja vyote vya ndege.

“Idadi ya mbwa inatakiwa iongezwe hasa inapokaribia kuhamia kwenye jengo jipya la tatu la abiria, ambalo litakuwa na idadi kubwa ya abiria na changamoto nyingi, pia kwa viwanja vingine navyo vitaangaliwa kwa suala la ulinzi,” alisema Masauni.

Hatahivyo, amesema hatasita kukifuta kitengo cha mbwa endapo hakutakuwa na mbwa wa kukidhi mahitaji na wenye sifa zote, kwani kwa sasa askari binadamu ni wengi zaidi.

Ametoa maelekezo kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi  (IGP), Simon Sirro  kuhakikisha mfumo na ushiriki wa askari wake unaweza kuboreshwa na wale wanapelekwa viwanja vya ndege wawe na sifa na vigezo maalum vya kuweze kubaini vitu kama nyara za serikali, madini na  madawa ya kulevyia.

“Hii itasaidia kwa kuwa na mfumo wa pamoja wa ushirikiano katika udhibiti, jingine ni kuhakikisha IGP analisimamia na kulitekeleza kwa haraka sana, kwani tumekuwa na askari mbwa waliopata mafunzo maalum ya kubaini vitu mbalimbali vinavyopitishwa kwenye viwanja vya ndege, hivyo maelekezo yangu kwake tuongeze idadi ya mbwa wenye sifa hapa JNIA ili kufanya kazi kwa ufanisi zaidi,” alisema Masauni.

Masauni amefanya ziara hiyo siku moja baada ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kushughudia makabidhiano ya kilo 35.267 za dhahabu zilizokamatwa Februari 15, 2019 katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Jomo Kenyatta, Nairobi nchini Kenya.

Saturday 27 July 2019

Real Yakiona cha Mtema Kuni, Yachapwa 7-3

Diego Costa, mfungaji wa bao nne pekee wakati Real Madrid ikifungwa 7-3 na Atletico Madrid.

NEW JERSEY, Marekani
DIEGO Costa alifunga mabao manne na alitolewa wakati Atletico Madrid ikiisambaratisha Real Madrid kwa mabao 7-3 jijini hapa.

Costa alifungua ukurasa wa mabao katika dakika ya kwanza na kukamilisha hat-trick yake kwa bao la penalti alilofunga katika dakika ya 45.

Joao Felix, mchezaji aliyesajiliwa katika kipindi hiki cha majira ya joto kwa ada ya  pauni milioni 113, naye pia alifunga bao lake la kwanza katika klabu hiyo wakati Atletico ikiongoza kwa mabao 5-0 hadi mapumziko.

Costa alingeza la nne dakika sita baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, kabla ya yeye na mchezaji wa Real Dani Carvajal hawajatolewa kwa kadi nyekundu baada ya kupigana katika dakika ya 61.

Angel Correa, aliyeingi aakichukua nafasi ya majeruhi Alvaro Morata, naye pia alizifumania nyavu katika kipindi cha kwanza, wakati Vitolo alifunga bao la saba kwa Atletico katika dakika ya 70.

Real waliendelea kuwa nyuma kwa mabao 6-0 kabla Real Madrid haijarekea katika ubao wa matangazo kwa mabao kupitia kwa Nacho, wakati Karim Benzema na Javier Hernandez wote wakifunga mabao katika dakika za majeruhi.

Gareth Bale, ambaye anajiandaa kuondoka Real Madrid na kujiunga klabu ya China ya Jiangsu Suning, alianzia katika benchi, lakini aliingia katika dakika 30 za mwisho.

Real, ambayo ilitumia kiasi cha pauni milioni 300 katika kipindi cha majira ya joto, ilianza kusajili kwa kumsajili Eden Hazard na Luka Jovic.

Lakini walipambana katika ziara yao ya Marekani kabla ya kuanza kwa ligi, ambapo walifungwa 3-1 na Bayern Munich na kuifunga Arsenal kwa penalti baada ya kutoka sare ya 2-2.

"Tulipoiangalia Madrid, tulikuwa tukiangalia wapi tutaimaliza, “alisema kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone. "Tulikuwa na muda mzuri hapa.”

Nahodha wa Real Sergio Ramos alisema: "Ni wazi hatuikuwa tukijisikia vizuri hapa. Na huu ndio mwanzo wa maandalizi yetu, Kuna njia nyingi zinazokufanya ushindwe, lakini hatuwezi kufanya kama tulivyofanya leo.

Kocha wa Real Zinedine Zidane aliongeza: "Hatuna haja ya kumtafuta mchawi katika hilo, hii ni mechi za maandalizi kabla ya kuanza kwa msimu mpya.


Bale Kulamba Bil 2.4 Kwa Wiki Akicheza China

MADRID, Hispania
GARETH Bale anakaribia kukamilisha uhamisho kutoka Real Madrid kwenda katika klabu ya China ya Jiangsu Suning kwa mkataba wa miaka mitatu utakaomuwezesha kuweka kibindoni mshahara wa pauni milioni 1 (sawa na sh bilioni 3) kwa wiki.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Wales, yuko katika hatua za mwisho za makubaliano na Jiangsu, ambao sasa wana uhakika wa kukamilisha usajili wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30.

Endapo mpango huo utakwenda vizuri, basi Bale atakuwa amelamba dume kwa kupata karibu mara mbili ya mshahara wake wa pauni 600,000 kwa wiki ambao analipwa Real Madrid na atakuwa nyota mkubwa kujiunga na Ligi Kuu ya China.

Klabu ya Beijing Guoan nayo pia imeulizia kutaka kumsajili, lakini Jiangsu ndio inaonekana kushinda mbio hizo za kumpata mchezaji huyo.

Lionel Messi ndiye mchezaji soka anayelipwa zaidi duniani, ambapo kwa wiki anaondoka na karibu pauni milioni 1.7 katika Barcelona, na mkataba wa Bale pale  Jiangsu utamuwezesha kumkaribia mchezaji huyo wa Barca.

Chanzo cha karibu kabisa na mchezaji huyo wazamani wa Tottenham Hotspur kimeelezea ofa hiyo ya Jiangsu kama ni “isiyoelezeka”.

Bale alikuwa akijiandaa kung’ang’ania kubaki Real Madrid, licha ya kocha Zinedine Zidane kuweka wazi kuwa anamtaka mchezaji huyo kuondoka katika klabu hiyo, lakini taarifa zilizotolewa na Telegraph Sport, zinasema mchezaji huyo yuko tayari kwenda China.

Chanzo kutoka Hispania kinadai kuwa Bale atasaini mkataba wa miaka mitatu ndani ya saa kadhaa, ingawa marafiki wa mchezaji huyo Ijumaa walisema mpango huo bado haujakamilika vizuri.

Zidane alimaliza kipindi cha Bale Real Madrid baad aya mchezo wa kirafiki wa maandalizi uliofanyika Jumapili iliyopita dhidi ya Bayern Munich aliposema: 
“Hajamuhusisha mchezaji huyo katika kikosi chake wakati klabu hiyo ikifanyia kazi suala la kuondoka kwake, na ndio maana hakucheza.

“Tutaangalia nini kitatokea katika siku zijazo. Tunatakiwa kuangalia nini kitatokea kesho, endapo kitatokea, basi ni jambo zuri. Acha tuwe na matumaini kwa faida ya kila mmoja, na hilo litatokea haraka sana. Klabu inawasiliana na klabu nyingine…”

Wakala wa Bale, Jonathan Barnett aliendelea kusema kuwa Zidane “amekywqa amuheshimu” mteja wake, lakini kocha huyo ameendelea kusisitiza kuwa hali ya mshambuliaji hyo bado inabaki vile vile licha ya Marco Asensio kuendelea kuwa majeruhi kwa muda mrefu.

Zidane pia aliendelea kumbania Bale, huku akiendelea kuwa kimya bila kuelezea mcheaji huyo anataka nini.

Sasa inaonekana kipindi cha miaka sita cha Bale kukaa Real kimekaribia kumalizika na kuiacha klabu hiyo aliyotwaa nayo mataji manne ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na taji la La Liga.

Hiyo inamfanya Bale kuwa mwanasoka wa Uingereza mwenye mafanikio zaidi anayecheza soka nje hasa pale aliponunuliwa kwa rekodi ya ada ya pauni milioni 85 wakat akitua Real akitokea Tottenham mwaka 2013.

Dirisha la usajili China linatarajia kufungwa Jumatano ijayo, lakini Bale anatarajia kuwa mchezaji wa Jiangsu katika kipindi hicho na kuhamia kwake China kutamfanya kupata mapokezi ya kishujaa.

Kwa sasa Ezequiel Lavezzi ndiye mchezaji anayelipwa zaidi China kwa anapewa pauni 500,000 kajubu mkataba wa Bale utafunika huo wa Muargentina huyo.

Ni Kisasi Taifa Stars, Harambee Leo Uwanja wa Taifa

Wachezaji wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, wakijifua kwenye Uwanja wa Boko Veterani.

Na Mwandishi Wetu
TIMU ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ inatarajiwa kucheza kesho dhidi ya timu ya taifa ya Kenya ‘Harembee Stars’ mchezo wa kwanza wa kutafuta tiketi ya kufuzu fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan 2020) utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mchezo huo ni muhimu kwa Stars kuhakikisha inatumia vyema uwanja wa nyumbani kupata matokeo mazuri ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga raundi ya mwisho ya kufuzu. Timu hizo zitarudiana Agosti 4.

Stars inataka kulipiza kisasi hasa baada ya kufungwa katika mchezo wa makundi kwenye fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon 2019) Misri bada ya kuchapwa 3-2 licha ya kuongoza mara mbili.

Lakini mchezo wa leo utawahusisha wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani na Taifa Stars ndio inaonekana kuwa na faida zaidi baada ya kuwa na asilimia kubwa ya kikosi chake kilichoenda Misri kupata uzoefu mkubwa.

Iwapo watatumia vyema uwanja wa nyumbani watajitengenezea mazingira mazuri ya kufuzu.

Hatahivyo, Kenya sio timu ya kubeza kwani wako vizuri na wanataka kuutumia mchezo huo kupata matokeo ili kujiweka vizuri kwa ajili ya mchezo wa mwisho utakaofanyika Nairobi wiki ijayo.

Katika viwango vya ubora wa soka duniani bado Kenya wako vizuri ukilinganisha na Tanzania, wanashikilia nafasi ya 107, huku ndugu zao wakishika nafasi ya 137.
Kila mmoja ana nafasi ya kupata matokeo kulingana na alivyojiandaa dhidi ya mpinzani wake kimbinu.

Mchezo huo utakuwa ni mtihani wa kwanza kwa makocha Ettiene Ndayiragije na wenzake walioteuliwa kukaimu nafasi ya Emmanuel Amunike na Hemed Morocco.
Akizungumzia mchezo huo Kocha Ndayiragije alisema alisema jana kuwa maandalizi yote yako vizuri na kwamba kinachohitajika kwa wachezaji ni umakini kuhakikisha wanapata matokeo mazuri.

Nahodha John Bocco alisema mchezo huo utakuwa mgumu kwani kila mmoja atahitaji matokeo kujiweka katika nafasi nzuri, lakini anaamini kwa morali walionao watapambana kupata matokeo mazuri kwenye uwanja wa nyumbani.

Bocco aliwaomba Watanzania kutoenda uwanjani na matokeo yaliyopita bali sasa wako vizuri kulipiza kisasi kwa kuhakikisha wanapata ushindi katika mchezo huo.

Tanzania kwa mara ya mwisho ilishiriki fainali za Chan zilipofanyika Ivory Coast 2009 ikiwa ni miaka 10 sasa, hivyo itataka mwaka huu iweke rekosi tena kwa kufuzi fainali hizo.

Fainali za kwanza za Chan zilifanyika mwaka 2009 na lengo la Shirikisho la Afrika (Caf) ni kutoa nafasi kwa wachezaji ambao hawajasajiliwa nje ya nchi zao na kuwawezesha kujitangaza.

Ulinzi Kuimarishwa Viwanja vya Ndege Tanzania


 
 Mhandisi Burton Komba (wanne kulia) anayesimamia mradi wa ujenzi wa Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TB3), akimweleza jambo Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani nchini, Hamad Masauni  (mwenye suti) alipotembelea jengo hilo hivi karibuni.


Na Mwandishi Wetu

Wizara ya Mambo ya Ndani nchini, itaongeza askari watu na mbwa kwa ajili ya kuimarisha ulinzi na usalama kwenye viwanja vya Ndege nchini.

Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Hamad Masauni amesema hayo alipofanya ziara ya kikazi katika Jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA TB3).

Masauni amesema serikali inatarajia kuongeza askari mbwa wengi wenye mafunzo na sifa, ili kuongeza ufanisi na ulinzi wa viwanja vyote vya ndege.

“Idadi ya mbwa inatakiwa iongezwe hasa inapokaribia kuhamia kwenye jengo jipya la tatu la abiria, ambalo litakuwa na idadi kubwa ya abiria na changamoto nyingi, pia kwa viwanja vingine navyo vitaangaliwa kwa suala la ulinzi,” alisema Masauni.

 Ofisa Usalama Mwandamizi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Ramadhani Mkumbukwa (aliyenyoosha mkono), akimweleza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni (wapili kulia) namna ya ukaguzi wa abiria na mizigo unavyofanyika wakiwa kwenye jengo la tatu la abiria la JNIA hivi karibuni.

Hatahivyo, amesema hatasita kukifuta kitengo cha mbwa endapo hakutakuwa na mbwa wa kukidhi mahitaji na wenye sifa zote, kwani kwa sasa askari binadamu ni wengi zaidi.

Ametoa maelekezo kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi  (IGP), Simon Sirro  kuhakikisha mfumo na ushiriki wa askari wake unaweza kuboreshwa na wale wanapelekwa viwanja vya ndege wawe na sifa na vigezo maalum vya kuweze kubaini vitu kama nyara za serikali, madini na  madawa ya kulevyia.

“Hii itasaidia kwa kuwa na mfumo wa pamoja wa ushirikiano katika udhibiti, jingine ni kuhakikisha IGP analisimamia na kulitekeleza kwa haraka sana, kwani tumekuwa na askari mbwa waliopata mafunzo maalum ya kubaini vitu mbalimbali vinavyopitishwa kwenye viwanja vya ndege, hivyo maelekezo yangu kwake tuongeze idadi ya mbwa wenye sifa hapa JNIA ili kufanya kazi kwa ufanisi zaidi,” alisema Masauni.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni (mwenye suti), akionyesha jambo akiwa kwenye eneo la ukaguzi wa abiria na mizigo wakati alipotembelea jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa la Julius Nyerere (JNIA TB3) hivi karibuni.
Masauni amefanya ziara hiyo siku moja baada ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kushughudia makabidhiano ya kilo 35.267 za dhahabu zilizokamatwa Februari 15, 2019 katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Jomo Kenyatta, Nairobi nchini Kenya.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni (kulia) akiongozana na maafisa wa ulinzi na usalama kukagua sehemu za kupitisha mizigo kwenye Jengo la tatu la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa la Julius Nyerere (JNIA TB3), alipofanya ziara hivi karibuni.


Thursday 18 July 2019

STARS YAPANGWA NA TUNISIA, LIBYA NA GUINEA YA IKWETA MBIO ZA KUFUZU AFCON 2021 CAMEROON


CAIRO, Misri
TIMU ya taifa ya Tanzania imepangwa katika Kundi J pamoja na Tunisia, Libya na Guinea ya Ikweta, katika mbio za kuwania kufuzu kwa fainali zijazo za michuano ya Mataifa ya Afrika zitakazofanyika Cameroon 2021.

Hilo limebainka baada ya Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) kupanga ratiba hiyo katika hafla iliyofanyika jijini hapa.

Katika kundi hilo la Tanzania na Tunisia ndizo pekee zilikuwepo katika fainali za mwaka huu ambazo zinamalizika kesho jijini hapa, kwa kuzikutanisha Algeria na Senegalm ambazo zote zimetoka katika Kundi C pamoja na Tanzania, huku Guinea ya Ikweta na Libya zilishindwa kufuzu.

Tunisia wenyewe ilifungwa na Nigeria 1-0 jana katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu Afcon 2019 Misri wakati Tanzania ilifungwa mechi zote tatu za Kundi C, ikiwa  2-0 na Senegal, 3-2 na Kenya huku Algeria ikiichapa Stars 3-0.
Kenya iliyokuwa kundi moja na Tanzania kwenye fainali za mwaka huu, yenyewe kwenye mbio za kusaka tiketi ya kwenda Cameroon 2021, imepangwa Kundi G pamoja na wenyeji wa mwaka huu Misri, Togo na Comoro.

Uganda wamepangwa Kundi B pamoja na Burkina Faso, Malawi na ama Sudan Kusini au Shelisheli, wakati Algeria imepangwa Kundi H pamoja na Zambia, Zimbabwe na Botswana na Senegal ipo Kundi I pamoja na Kongo, Guinea Bissau na Eswatini.

MAKUNDI YOTE KUFUZU AFCON 2021 CAMEROON

Kundi A: Mali, Guinea, Namibia, Liberia/Chad

Kundi B: Burkina Faso, Uganda, Malawi, Sudan Kusini/Shelisheli

Kundi C: Ghana, Afrika Kusini, Sudan, Mauritius/Sao Tome

Kundi D: DRC, Gabon, Angola, Djibouti au Gambia

Kundi E: Morocco, Mauritania, CAR, Burundi

Kundi F: Cameroon, Cape Verde, Msumbiji, Rwanda

Kundi G: Misri, Kenya, Togo, Comoro

Kundi H: Algeria, Zambia, Zimbabwe, Botswana

Kundi I: Senegal, Congo, Guinea Bissau, Eswatini

Kundi J: Tunisia, Libya, Tanzania, Equatorial Guinea

Kundi K: Ivory Coast, Niger, Madagascar, Ethiopia

Kundi L: Nigeria, Benin, Sierra Leone, Lesotho