Tuesday 30 May 2017

Viongozi wapya Tava kupatikana Julai 8 Moshi

Makamu mwenyekiti wa Tava, Muharami Mchume.
Na Mwandishi Wetu
UCHAGUZI Mkuu wa Chama cha Mpira wa Wavu Tanzania (Tava) umepangwa kufanyika Julai 8 mjini Moshi.

Kamati ya Utendaji ya Tava ilikutana juzi na kumalizika kikao chao usiku, ambapo walikubaliana kuwa uchaguzi huo ufanyike Moshi tarehe hiyo.

Makamu mwenyekiti wa Tava, Muharami Mchume alisema juzi kuwa, mikoa imetakiwa kufanya chaguzi zao mapema kabla ya huo wa taifa.

Alisema kuwa mikoa ambayo haijafanya chaguzi zao na kusajiliwa, kamwe haitaruhusiwa kuingia katika Uchaguzi Mkuu wa Tava.

Alizitaja nafasi zigakazogombewa kuwa ni mwenyekiti, makamu mwenyekiti wa kwanza anashughuliwa mipango na maendeleo, makamu wa pili anashughulikia fedha na utawala, katibu mkuu na katibu msaidizi.

Nafasi zingine ni zile za mwenyekiti wa kamisheni ya wavu wa ufukweni, Maendeleo ya Mikoa, kamiosheni ya Makocha, Waamuzi pamoja na ile ya Wanawake na Watoto.

Mchume alisema kuwa uchaguzi huo utasimamiwa na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na tayari fomu za uongozi zimeanza kutolewa kwa wale wanaotaka kuwania nafasi hizo.


Wale wanaotaka kugombea nafasi za juu, watanunua fomu kwa sh 100,000 wakati viongozi wa kamishneni kila fomu itauzwa sh 50,000.

Geay, Huche wang'ara mbio Marekani, Ufaransa

Na Mwandishi Wetu
WANARIADHA wa Tanzania wameng’ara katika mbio mbalimbali za kimataifa nje ya nchi baada ya kushika nafasi ya kwanza na ya tatu.

Gabriel Geay alimaliza wa kwanza katika mbio za kimataifa za kilometa 10 za Marekani za Bolder Boulder kwa kutumia dakika 29:02:19 na kutwaa jumla ya dola za Marekani 8,000 (sawa na sh 17,904,000).

Mbio hizo za Marekani zilishirikisha zaidi ya wakimbiaji 50,000 kutoka duniani kote, huku kitimu, Tanzania ilishika nafasi ya nne.

Wanariadha wengine wa Tanzania walioshiriki mbio hizo na nafasi walizoshika ni pamoja na Ismail Juma (18) aliyetumia dakika 30:43:99 na Josephat Joshua (20) kwa dakika 30:58:17.

Wanariadha hao ndio walikuwa wakiunda timu ya Tanzania iliyoshika nafasi ya nne na kuondoka na dola za Marekani 6,000 wakati ushindi binafsi wa Geay umempatia dola 3,000 na pia amelamba bonasi ya dola 3,000 kutoka kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas.

Wachezaji hao watatu wakagawa zawadi ya dola 6,000, amapo kila mmoja ataondoka na dola za Marekani 2,000.

Kwa mujibu wa Katibu wa Riadha Tanzania (RT), wachezaji hao watarejea leo jijini Dar es Salaam na kukatisha ziara yao katika chuo kikii komoja cha Marekani baada ya Juma kuugua ghafla.

Aidha, mwanariadha mwingine wa Tanzania, Stephano Huche mwishoni mwa wiki aling’ara katika mbio za marathoin za Saint Michel zilizofanyika nchini Ufaransa baada ya kumaliza wa pili kwa kutumia saa 2:15:26.
Huche amefunzi kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya dunia ya riadha yatakayofanyika London, Uingereza Agosti akiungana na akina Alphonce Felix, Said Makula, Fabian Joseph na Jaffer Ngimba.

Multichoice Tanzania yasheherekea Siku ya Afrika

Kwa kipindi kizima cha mwezi wa  Mei wateja wa DStv wamekuwa wakifurahia zaidi vipindi  vyenye ubora na vya kusisimua  vya Kiafrika.

Huba, Jikoni na Marion, Mchikicho wa Pwani, Yahusu Tanzania, Kimbembe ni kati ya vipindi kutoka Tanzania vilivyo bamba mwezi huu ndani ya chaneli ya Maisha Magic Bongo (DStv 160)
Meneja Mahusiano Multichoice Tanzania, Johnson Mshana amesema, “Mwezi Mei kwetu tumeufanya kuwa mwezi maalum kwa ajili ya kutangaza na kujivunia  utajiri wetu  waafrika ikiwa ni pamoja na utamaduni na Sanaa na michezo

Hii ni moja ya sehemu ya ahadi ya  DStv kwa kutoa ushirikiano kwenye  sekta ya sanaa na burudani kwa kuendelea kusaidia Filamu za Afrika na kwa kuwekeza katika watu, mawazo na vipaji.
Ikiwa ni njia moja wapo ya kusheherekea mwezi huu wa Afrka, Wafanyakazi  wa Multichoice Tanzania waliamua kuvaa mavazi maalum ya Kiafrika na kuandaa chakula maalum cha kiafrika kwa wafanyakazi wote.
Haikuishia hapo, Multichoice Tanzania pia imeandaa zawadi maalum za Kiafrika kwa waandishi wa habari, ikiwa ni njia ya kuonesha shukrani kwa waandishi na kudumisha Umoja na Uafrika wetu.

AFRIKA YETU

 Johnson Mshana| PR Manager
Telephone: +255784557755

Email: Johnson.Mshana@tz.multichoice.com

Saturday 27 May 2017

Wanariadha wa Tanzania kulamba mamilioni Marekani katika mbio za Bolder Boulder


Na Mwandishi Wetu
WANARIADHA wa Tanzania, Josephat Joseph, Ismail Juma na Gabrie Gerald watalamba kitita cha Dola za Marekani 15,000 (sawa na Sh 33,540,000) endapo watashinda mbio za kilometa 10 za Bolder Boulder zitakazofanyika Jumatatu Marekani.

 Waandaaji wa mbio hizo wameandaa kiasi cha dola za Marekani 42,000 (sawa na Sh milioni 94) ikiwa ni zawadi kuanzia mshindi wa kwanza hadi wa tano kwa wanaume na wanawake. 
Wanariadha wawili wa Tanzania, Joseph na Juma waliondoka nchini juzi kupitia Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Kilimanjaro kwenda Colorado, Marekani ambako wataungana na Gerald kwa ajili ya mashindano hayo.

 Taarifa za mtandao zilisema kuwa dola 15,000 zinatolewa kwa timu itakayoshinda ambayo itakuwa na wanariadha watatu huku zawadi binafsi kwa mshindi wa kwanza ni dola 3,000. 

Kwa mujibu wa waandaaji, mbio hizo ndizo hutoa zawadi za fedha nyingi kuliko mbio zozote zisizo za marathoni Marekani, ambapo hutoa kiasi cha dola 10,800 katika zawadi binafsi kwa ajili ya washindi 10 wa kwanza. 
Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania, Wilhelm Gidabuday alisema juzi kuwa vijana hao baada ya mbio hizo wanatarajia kutembelea katika Chuo Kikuu cha Adam State kilichopo Almos katika Jimbo la Colorado, Marekani.
Rekodi ya mashindano hayo kwa upande wa wanaume ni muda wa dakika 27:52 wakati ile ya wanawake ni 32:13, ambapo mwanariadha atakayemaliza katika muda mzuri zaidi, atapata bonasi itakayojumuishwa na zawadi za washindi.

Simba mabingwa wapya Kombe la FA 2017

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
SIMBA ya Dar es Salaam leo imekata tiketi kupanda ndege baada ya kutwaa taji la Kombe la FA kufuatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mbao FC katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini hapa.

Simba iliandika bao la kwanza katika dakika ya 95 ikiwa ni dakika tano tangu muda wa nyongeza uanze, lililofungwa na Fredricka Blagnon aliyeingia akitokea benchi na kuzua shamra shamra kwa wapenzi wa Simba.

Mbao FA walisawazisha bao hilo kupitia kwa Ndaki Robert katika dakika ya 110 baada ya mabeki wa Simba kufikiri kuwa mfungaji ameotea.

Simba walipata penalti katika dakika ya 121 baada ya mchezaji mmoja wa Mbao FC kuunawa mpira katika eneo la hatari baada ya kutokea piga nikupige na Shizza Kichuya alifunga penalti hiyo.

Kwa taji hilo, Simba sasa itapata nafasi ya kuliwakilisha taifa katika mashindano ya Kombe la 
Shirikisho Afrika msimu ujao.

Pius Buswuta wa mbao alikosa bao katika dakika ya nne akiwa ndani ya eneo la hatari, alipiga nje mpira huo.

Simba ilinusurika kufunga mara baada ya kuanza kwa kipindi cha pili wakati Kichuya akiwa katika nafasi nzuri ya kufunga, alishindwa kufanya hivyo baada ya Yussuf Ndukumana kuokoa.

Juuko nusura afunge lakini alikosa bao baada ya kupiga kichwa na mpira kupanguliwa na kipa wa Mbao FA, Benedict Haule.

Nafasi hii inaiwezesha Simba kupanda ndege baada ya kushindwa kufanya hivyo kwa takribani miaka minne baada ya kuzikosda nafasi mbili za kwanza na kuwafanya kutoshiriki mashindano ya kimataifa.

Kwa mara ya mwisho Simba ilishiriki mashindano hayo ya kimataifa ni Februari 17, 2013 walipofungwa mabao 4-0 na DC Libolo ya Angola katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika.

Karibu miaka yote minne, Yanga na Azam ndio walikuwa wakipokezana nafasi ya kwanza na pili.
Mbao FC pamoja na kucheza mara ya kwanza Ligi Kuu pamoja na fainali hiyo ya FA, lakini ni timu imara hasa ukizingatia ilizifunga Yanga, Azam FC, Kagera Sugar na Mtibwa Sugar katika ligi.

Kwa muda mrefu Simba imekuwa ikiitwa wa matopeni huku Yanga ikiwa ya kimataifa kufuatia timu hiyo kushindwa kufuzu kwa michezo ya kimataifa wakati watani zao walikuwa wakifuzu kila mwaka na kufanikiwa kupanda ndege.

Vikosi vilikuwa Simba: Daniel Agyei, Jamvier Bukungu, Mohamed Hussein, Juuko Murshid, James Katei, Jonas Mkude, Shiza Kichuya, Mzamini Yasin, Laudit Mavugo, Said Ndemla/Fredricka Blagnon na Juma Luizio/Ibrahim Ajibu.

Mbao FC: Benedict Haule, David Mwasa, Salimin Hoza, Asante Kwasi, Boniface Maganga, Yussuf Ndikumana, George Sangija/Dickson Ambundo, Jamal Mwambeleko, Pius Buswita, Habibu Haji/Rajishi Kotecha na Ibrahim Njohole.

Friday 26 May 2017

Lukaku kukipiga Dar es Salaam akiwa na Everton

Na Mwandishi Wetu
KLABU ya Everton ya England inatarajia kuzuru Tanzania kucheza mechi za kujiandaa na msimu mpya wa 2017/18, tovuti ya klabu hiyo imeandika.

Taarifa hiyo imeandika Everton watatembelea Tanzania na itakuwa timu ya kwanza ya Ligi Kuu ya England kucheza mechi katika nchi za Afrika Mashariki.

Ziara hiyo ambayo itakuwa sehemu ya sherehe zao za udhamini mpya wa Kampuni ya SportPesa, itaifikisha Everton kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wenye uwezo wa kubeba mashabiki 60,000 kucheza mechi Alhamisi ya Julai 13.

Tanzania na Kenya zitakutanisha timu nane, nne kutoka kila upande katika michuano ya SportPesa, kuwania nafasi ya kucheza Romelu Lukaku.

Mapema mwezi huu, Everton ilitangaza udhamini mnono wa rekodi na SportPesa wa miaka mitano na baada ya hapo kampuni hiyo ikaingia Afrika Mashariki kuingia mkataba na klabu kadhaa kubwa, zikiwemo Simba na Yanga.

Michuano ya SportPesa Super Cup inatarajiwa kuanza Juni 5 hadi 11 Dar es Salaam, ikishirikisha timu za Simba, Yanga, Singida United na Jang'ombe Boys za Tanzania, Gor Mahia, AFC Leopards, Nakuru All Stars na Tusker FC za Kenya.

Bingwa wa michuano hiyo itakayofanyika Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam ndiye atamenyana na Everton na pia ataondoka na kitita cha sh. milioni 60.


Everton imemaliza ya saba katika msimamo wa Ligi Kuu ya England ikijikusanyia jumla ya pointi 61 huku Chelsea ikimaliza ya kwanza kwa kuwa na pointi 93 katika ligi hiyo inayoshirikisha timu 20.

Katibu RT ampongeza Rais Magufuli

Uwizi huu upo tangu siku nyingi na kuna uwizi mwingine mwingi tu unaendelea.

Our problem is an illness called "Reluctant to take immediate action due to hate caused by political differences"

Ilishindikana nini kipindi kileeeee, ampapo Tundu Lissu alisema hayo hayo, Zitto Kabwe, Kafulila na wazalendo wengine?

Katika watanzania ambao hawakustuka hata tone kuhusu ripoti hii mimi ni mojawapo sababu THIS IS AN OLD STORY.

However, we've got to respect the new beginning dared by H.E Dr Magufuli / our President.

The question is - lini sasa serikali itaanza kudili na waonevu wengine kama - Waarabu wa Loliondo wanaobeba wanyama wetu, wababe waliovamia Vyanzo vya Maji ambao wanakausha mamilioni ya lita za ujazo wa RASILIMALI MAJI.

Ukizungumzia RASILIMALI usisahau MIFUGO wanaosafirishwa kinyemela kupitia Bandari Bubu za Bagomoyo kwa MPANGO mahsusi wa DC Bagamoyo na Maafisa wake wa POLISI. Kodi za serikali zinaangamizwa na wateule walioaminiwa.

Ripoti ya Bagamoyo imefichwa na kigogo mmoja wa Pwani (jina lake tunalihifadhi)  ili kulinda maslahi ambayo na yeye (anamtaja jina) anafaidika nayo.

Niliwahi kumwandikia barua Rais Magufuli (nakala) ipo, ilihusu ombi la wafugaji wa Bagamoyo ambao walitaka Rais afahamu kwamba; kwa moyo wa dhati wanataka wachange mamilioni yao, wajenge kiwanda cha nyama ili watengeneze ajira kwa majirani zao ambao wengi ni wakulima. Pia hiyo iwe ni njia bora ya kupunguza mifugo wakati serikali ikipata kodi ya mauzo ya mazao ya nyama, ngozi nk.

Lakini pia ilikuwa njia nzuri ya wao kupunguza mifugo, kubadili mtazamo wao wa kuanza kusomesha watoto wao, kujenga Nyumba bora nk.

Nahakika ujumbe huu ungemfurahisha sana Rais wetu, lakini nina uhakika barua hiyo Rais atakuwa hajaiona sababu mpango huo mzuri utapoteza ulaji wa hao wanaopora mifugo ya watanzania wanyonge na kusafirisha nje ya nchi bila kulipa kodi.

Bagamoyo ni hatari, serikali inaibiwa na kiongozi, alafu tena mwananchi anaporwa na kiongozi...!

Namhurumia Rais Magufuli sababu HE IS FIGHTING THIS WAR ALONE. Those who he trusted are conspiring against him; and when he finally finds out the truth - the damage has already been done.

Lastly, I salute what the Commander in Chief has achieved so far, I pray for his wellbeing because he is at war within his own 'Inner Circle'.

I wish you all a pleasant day.

By Gidabuday

May 25th 2017

RT yawashukuru wadau waliofanikisha mashindano ya Kanda ya Tano ya Afrika

Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania, RT, Wilhelm Gidabuday akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Tullo Chambo.
Na Mwandishi Wetu
RIADHA Tanzania (RT) imewashukuru wadau waliofanikisha kufanyika kwa mafanikio mashindano ya 12 ya riadha ya vijana wenye umri chini ya miaka 18 jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Tanzania ilikuwa mwenyeji wa mashindano hayo ya vijana yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa na Tanzania ilitwaa ushindi wa kwanza kwa upande wa wanawake huku ikishika nafasi ya pili katika ushindi wa jumla.
Katibu Mkuu wa RT, Wilhelm Gidabuday aliwashukuru wadau, kampuni na watu mbalimbali waliofanikisha kufanyika mashindano hayo ya vijana.

Gidabuday alisema kuwa mashindano hayo yalifanikiwa na kufanyika kwake kumewezesha wanariadha 17 wa Tanzania kufuzu kwa mashindano ya dunia yatakayofanyika Nairobi, Kenya Julai 12 hadi 16.
Alisema kama wadau wangeshindwa kujitokeza kusaidia kufanyika kwa mashindano hayo na RT ingeshindwa kuyaandaa, “basi wanariadha wetu wasingeweza kufuzu kwa mashindano hayo ya Dunia.”

Alisema Shirikisho la Kimataifa la Riadha (IAAF) limeipa Tanzania nafasi mbili tu ya kushiriki mashindano hayo, ambao itawagharamia, huku RT ikisaka fedha kwa ajili ya kuwagharamia wanariadha 15 waliobaki.
Aidha, Gidabuday alisema kuwa, RT pia itajitahidi kupeleka wanariadha wengi katika mashindano ya dunia ya wakubwa yatakayofanyika London, Uingereza Agosti.

Pia alisema kwa sasa wanasaka fedha kwa ajili ya kambi za timu hizo mbili, ya vijana na ile ya wakubwa ili kuhakikisha Tanzania inafanya vizuri katika mashindano hayo yote.
Wadhamini wa mashindano hayo ni NMB, PPF, Vodacom, Serengeti Marathon na Maji Uhai.

Tuesday 23 May 2017

Manji atangaza kuachia ngazi Yanga

Na Mwandishi Wetu
MWENYEKITI wa Yanga, Yusuf Manji ametangaza kuachia ngazi rasmi kuiongoza klabu hiyo, imefahamika.

Kwa mujibu wa Katiba, Yanga sasa itakuwa chini ya uongozi wa Makamu mwenyekiti wake, Clement Sanga hadi pale uchaguzi wa kuziba nafasi hiyo utakapofanyika.

Akielezea kujiuzulu kwa, Mani alisema kuwa ameamua kukaa pembeni ili kuwapisha wengine nao waiongoza klabu hiyo.

"Nimeamua nipumzike nipishe wengine waongoze, Yanga ni yetu sote nilipoingezewa muda tu kwa demokrasia, lakini haimanishi kuwa Mimi ndio nitakua Mwenyekiti milele, " alisema Manji ambaye hata hivyo si mara yake ya kwanza kutangaza kuachana na klabu hiyo.

Agosti mwaka jana pia alitangaza kujiuzulu  ikiwa ni siku chache tangu alipotangaza kutaka kuikodi timu hiyo kwa muda wa miaka 10, huku asilimia 75 za timu hiyo zikiingia kwake na kutoa asilimia 25 kwa timu hiyo kila mwaka kitu kilichopingwa na wadau wengi wa Soka ikiwemo Serikali.

Hata hivyo, wanachama wa klabu hiyo walimpigia magoti na kumsihi asitishe azma yake hiyo, ambayo alikubali kuendelea na uongozi hadi juzi Jumamosi alipoijulisha rasmi kamati yake ya utendaji kuwa ni muda muafaka kwa yeye kukaa pembeni.

"Nia yangu yakujiuzulu ni ya muda mrefu, sikutaka kufanya maamuzi katikati ya ligi ningewachanganya wachezaji, nashukuru tumetetea ubingwa wetu naiacha Yanga ikiwa na kikosi bora na hata makocha pia.

" Yapo mengi mazuri ninayojivunia Yanga ikiwemo umoja na mshikamano, ikumbukwe nilingia wakati kuna mgogoro mkubwa, nikafanikiwa kumaliza hivyo ni muda sahihi na muafaka kwa Mimi kukaa pembeni.

Ikumbukwe Yanga ni klabu ya wanachama, Yanga ni kubwa kuliko mtu yoyote, naamini watakaofuatia wataendeleza pale nilipoishia, " alisisitiza.

Kwa upande wa Katibu wa Yanga Charles Mkwasa akizungumzia hilo alisema "Nimeona taarifa ya Mwenyekiti wetu kwenye mitandao, na nilikuwa nawasiliana naye kila siku kwa email na hajawahi kunieleza hili, ila kama kweli ni maamuzi yake basi tutayaheshimu," alisema.


Hatahivyo, kuondoka kwa Manji kunaweza kukawa si pigo sana kwa klabu hiyo ya Jangwani ambayo tayari imesaini mamilioni ya fedha kwa kudhaminiwa na Sports Pesa huku ikielezwa kuwa kuna makampuni kadhaa ambayo yapo mbioni kudhamini timu hiyo ya mtaa wa Twinga na Jangwani.

Monday 22 May 2017

Wanafunzi wa Filbert Bayi wafanyiwa tafrija nzito kwa kutwaa medali Kanda ya Tano Riadha

Mwenyekiti wa shule za Filbert Bayi, Filbert Bayi akiwa na wanafunzi wa shule hizo baada ya tafrija ya wanafunzi hao baada ya kufanya vizuri katika mashindano ya Kanda ya Tano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya umri wa miaka 18 juzi Kibaha mkoani Pwani.
Na Mwandishi Wetu
TAASISI ya Filbert Bayi (FBF) imesema kuwa itaendelea kugharamia elimu ya wanariadha watakaofanya vizuri katika michezo na masomo.

Hayo yalisemwa juzi na mwenyekiti wa shule hizo, Bayi wakati wa hafla ya kuwapongeza wanafunzi wa shule iliyowalioshiriki mashindano ya 12 ya riadha Kanda ya Tano ya Afrika.
Mashindano hayo ya vijana wenye umri chini ya miaka 18 yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuanzia Mei 13 na 14 mwaka huu.

Bayi alisema kuwa wataendelea kugharamia ada na mahitaji mengine yote ya wachezaji wenye vipaji ili waendelea kusoma katika shule hiyo iliyopo Mkuza Kibaha mkoani Pwani.

Katika mashindano hayo shule hiyo ilitoa wanariadha watano waliounda timu ya taifa ilishika nafasi ya pili kwa matokeo ya jumla huku ikimaliza ya kwanza kwa upande wa wasichana.

Wanafunzi wa shule hiyo walikuwemo katika timu ya taifa ya Tanzania iliyoshiriki mashindano hayo ni Rose Thesuni alipata medali tatu za dhahabu katkika mbio za meta 400, kuruka juu na zile za kupokezana vijiti za meta 4x400.

Thesuni alipata medali ya fedha katika mchezo wa kupokezana vijiti wa mbio za meta 4x400 huku Bitrina Alexander akipata medali moja ya dhahabu katika mbio za kupokezana vijiti za meta 4x100, medali ya fedha katika meta 4x400 na shaba katika meta 400.
Dorcus Ilanda mwenyewe alipata medali ya fedha katika mbio zakupokezana vijiti za meta 4x400 na medali ya shaba katika meta 800 wakati Regina Mpigachai akipata medali za fedha katika meta 800 na kupokezana vijiti 4x400.

Mwanariadha mwingine wa shule hiyo ni Esther Martin aliyeshiriki mbio za meta 3000 na kumaliza katika nafasi ya nne kwa kutumia dakika 10:23.18.
Mwanafunzi mmoja hugharimu kiasi cha sh milioni  1.6 kwa temu kwa mwanafunzi mmoja, ambapo kwa mwaka kila mwanafunzi anagharamiwa sh milioni 3.2.

Alisema kuwa pamoja na gharama kubwa lakini wataendelea kuwagharamia wanafunzi wenye vipaji ili kuviendeleza vipaji vyao katika mchezo huo.

Naye katibu msaidizi wa RT, Ombeni Zavalla aliipongeza FBF kwa kuwatunza watoto hao na kuwataka kuendelea kuwagharamia ili kuwajengea msingi wa maisha yao katika michezo na elimu.
Aliwataka wanafunzi hao kutumia muda wao vizuri kwa ajili ya masomo na michezo.

Thesuni aliyepata medali tatu za dhahabu na moja ya fedha alimshukuru Bayi kwa kuwawezesha kugharamiwa elimu na mahitaji mengine na kuahidi kuendelea kufanya vizuri kitaifa na kimataifa.

Wanafunzi hao walitwaa jumla ya medali 11, ambapo mbali na kukata keki katika hafla hiyo, pia walipewa zawadi ya fedha taslimu.



Sunday 21 May 2017

Yanga wapokewa kifalme wakitokea Mwanza

 







 

Arsenal yashindwa kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya

Mshambuliaji wa Everton, Kevin Mirallas (kulia) akikimbizwa na mchezaji wa Arsenal Alex Iwobi (katikati) wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya England leo kwenye Uwanja wa Emirates Jijini London. Arsenal ilishinda mabao 3-1.
LONDON, England
PAMOJA na kushinda mabao 3-1 dhidi ya Everton katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu ya England, Arsenal imeshindwa kufuzu kucheza Ligi ya Mabingwa wa Ulaya baada ya kumaliza  katika nafasi ya tano.

Timu hiyo ambayo ilianza siku ikiwa pointi moja nyuma ya Liverpool iliyokuwa katika nafasi ya nne, ilionekana kama ingeweza kumaliza ya nne baada ya kupata bao la kuongoza katika dakika ya nane.
Lakini Liverpool, ilihitaji ushindi tu wa aina yoyote ili imalize katika nafasi ya nne, ambapo ilianza kuifunga Middlesbrough kabla ya mapumziko na kuibuka na ushndi wa mabao 3-0.

Manchester City yenyewe ilimaliza ya tatu baada ya kupata ushindi rahisi wa mabao 5-0 dhidi ya Watford.

Ligi ya Ulaya kwa Arsenal

Hatua ya Arsenal kufuzu kucheza Ligi ya Ulaya kwa mara ya 19 mfululizo ilifikia tamati jana baada ya kumaliza katika nafasi ya tano.

Imani ilikuwepo kwa mashabiki wa nyumbani wakati Hector Bellerin alipoifungia the Gunners bao la mapema huku taarifa zikizagaa kuwa, Liverpool ilikuwa katika wakati mgumu dhidi ya wapinzani wao Hull City ambao tayari walishashuka daraja.
Kiungo wa Liverpool, Georginio Wijnaldum (kushoto) akiwania mpira pamoja na mchezaji wa Middlesbrough, Grant Leadbitter walati wa mchezo wa Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa Anfield mjini Liverpool, kaskazini magharibi ya England.
Liverpool sasa itacheza Ligi ya Mabingwa wa Ulaya kwa mara ya kwanza tangu ilipofanya hivyo kwa mara ya mwisho msimu wa mwaka 2014-15.

Manchester City ilitwaa nafasi ya tatu na kufuzu moja kwa moja kucheza hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya baada ya kushinda 5-0 dhidi ya Watford.

Mabingwa Chelsea imekuwa timu ya kwanza ya Uingereza kushinda mara 30 katika ligi kubwa katika mechi 38 za msimu mmoja wakati timu hiyo ikimuaga nahodha wao wa muda mrefu, John Terry huku ikipata ushindi mnono wa 5-1 dhidi ya Sunderland.

The Blues, ambayo imetwaa ushindi wake wa sita wa Ligi Kuu siku tisa zilizopita, ilijikuta nyuma baada ya bao la mapema la Javier Manquillo lakini ilijibu mapema kupitia Willian.

Eden Hazard alifunga bao lake la 17 la msimu na kuifanya timu yake kuongoza kabla nafasi yake haijachukuliwa na Pedro.

Katika mechi zingine za ligi hiyo, Burnley ilifungwa na West Ham mabao 2-1 huku Hull City ikipokea kichapo cha mabao 7-1 kutoka kwa washindi wa pili wa ligi hiyo, Tottenham.