Tuesday 10 March 2015

Timu za netiboli zaagwa, zatakiwa kuwa wazalendo


Baadhi ya wachezaji wa timu ya netiboli ya Uhamiaji wakati timu za tanzania zilipoagwa Uwanja wa Taifa kwa ajili ya mashindano ya Afrika Mashariki yatakayofanyika Zanzibar.


Na Seba Nyanga
TIMU za netiboli za JKT Mbweni, Uhamiaji Tanzania na JKT Ruvu zimeagwa leo na mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Dioniz Malinzi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Timu hizo ambazo zilikabidhiwa bendera na Malinzi zitashiriki mashindano ya Afrika Mashariki yatakayofanyika kisiwani Zanzibar kuanzia Jumamosi Machi 14.
Malinzi aliwakabidhi bendera ya taifa manahodha wa timu hizo, Zakia Kondo wa Uhamiaji, Panina Mayunga wa JKT Mbweni na Anitha Elius wa JKT Ruvu.
Mwenyekiti huyo wa BMT ambaye hii karibuni aliteuliwa tena kushika wadhifa huo kwa kipindi kingine cha miaka mitatu baada ya kumaliza kile cha mwanzo aliwataka wachezaji hao kwenda Zanzibar kushindana na si kushiriki.
Malinzi alisema kuwa ana usongo na mataji kwani katika kipindi chote cha uongozi wake ndani ya BMT hajawahi kuona medali, hivyo huu ni wakati wake wa kushuhudia ushindi.
Naye mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta) Annie Kibira aliwataka wachezaji wa timu hizo kuwa na umoja na kuacha maneno maneno.
Mtakakuwa Zanzibar mjitahidi sana kuwa wamoja kama wenzenu Wanzanzibar wanavyokuja huku na msiwe na idomo domo, alisema Kibira katika hafla hiyo iliyohudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa BMT Henry Lihaya.
mwenyekiti wa BMT Dioniz Malinzi akizungumza wakati wa kuziaga timu za Tanzania Bara zitakazoshiriki mashindano ya netiboli ya Afrika Mashariki yatakayoanza Jumamosi Zanzibar. Kushoto ni Katibu Mkuu wa BMT Henry Lihaya, kushoto kwa Malinzi ni mwenyekiti wa chaneta Annaie kibira na Judith ilunda mjumbe wa Chaneta.
Baadhi ya iongozi na wachezaji wa timu za Uhamiaji, JKT Mbweni na JKT Ruvu wakimskiliza mwenyekiti wa BMT (hayopo pichani0 wakati wakuziaga timu hizo.
 
Baadhi ya wachezaji wa timu ya Uhamiaji na JKT Mbweni wakichuana katika mchezo wa kirafiki jana kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, Uhamiaji   walishinda    




   

No comments:

Post a Comment