LONDON, England
MCHUMBA wa kipa wa Manchester United David de Gea
Edurne Garcia amekana madai kuwa Manchester sio mahali pazuri pakukaa,
akisisitiza kuwa, maneno hayo aliwekewa mdomoni na vyombo vya habari.
Uvumi kuwa De Gea yuko mbioni kuondoka Manchester
United ulizagaa mapema mwezi huu wakati wa mahojiano ya Garcia, aliyedaiwa
kutangaza kuwa hapendi kuishi katika jiji hilo.
'Sio mahali pazuri sana, huo ndio ukweli,' anasema Garcia
akijibu madai ya mtangazaji.
Lakini sasa, muimbaji huyo, atakayeliwakilisha Hispania
katika shindano la kuimba, alisisitiza kuwa maneno yake yalibadilishwa.
'Sijui kama walikuwa wakisaka habari au walitaka kuleta
utata, lakini ilinishangaza mimi wakati nilipoona sentensi hiyo kila mahali
ambayo kamwe si kuisema. Nafurahishwa na Manchester, naipenda, na ni mji wa
aina yake.'
Siku mbili baada ya mahojiano Meya wa Halimashauri ya
Jijini la Manchester Pat Karney alimkaribisha Garcia katika ziara ya kuzunguka
jiji ili kuona hali halisi.
Garcia anakiri kuwa amefurahi kuzungushwa katika jiji
hilo.
No comments:
Post a Comment