PARIS, Ufaransa
MCHEZAJI Zlatan Ibrahimovic alifunga mabao matatu pekee
yake `hat-trick’
wakati Paris St-Germain ikiifunga Lorient 3-1 na kushika uongozi wa Ligue 1.
Msweden huyo
alifunga penati mapema baada ya kufanyiwa madhambi na kipa wa timu
pinzani Benjamin Lecomte.
PSG ilitawala mchezo huo na bado ilikosa nafasi kadhaa
kabla Jordan Ayew hajasawazisha kwa shuti la umbali wa kama mita 20 na muda
mfupi baadae alikosa bao baada ya shuti lake kuzuiwa.
Lakini Ibrahimovic alifunga la pili kwa penati baada ya
kuchezewa vibaya na Javier Pastore na dakika za majeruhi alipachika bao la
tatu.
Mshambulijai huyo hivi karibuni alikuwa anawekwa benchi
kimakosa. Wiki iliyopitaalitolewa nje walipocheza dhidi ya Chelsea katika
mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya, hivyo amefungiwa mchezo mmoja na atakosa
mechi dhidi ya Barcelona.
Lakini uongozi huo wa PSG unaweza kuwa ni wa muda tu
endapo Lyon iliyokuwa ikikalia kiti hicho leo Jumamosi itaibuka na ushindi
dhidi ya Nice.
No comments:
Post a Comment