Friday 6 March 2015

Maandalizi mkutano wa Katiba RT yako poa




Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania, Suleiman Nyambui.
Na Mwandishi Wetu
MAANDALIZI ya mkutano maalum wa kujadili mabadiliko ya Katiba ya Riadha Tanzania (RT) utakaofanyika mjini Morogoro Aprili 14, yamepamba moto.

Katibu Mkuu wa RT Suleiman Nyambui alisema kuwa, maandalizi ya mkutano huo yamefikia pazuri na utafanyikia katika hoteli ya Nane Nane ulipofanyikia ule wa mwaka juzi.

Awali, mkutano huo ulifanyika mwaka juzi, lakini uliahirishwa baada ya wajumbe wengi kudai kuwa walichelewa kupelekea nakala ya rasimu hiyo ya Katiba.

Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Dioniz Malinzi ndiye aliyesimamia mkutano huo na kuamuru uahirishwe ili kutoa muda zaidi kwa wajumbe kupitia nakala hizo.

Nyambui alisema kuwa nakala hizo walizituma mapena na akishangaa kuona wajumbe wakidai kuwa walichelewa kupelekewa.

Alisema kuwa ni matarajio yake kuwa mkutano wa mwaka huu utakwenda vizuri na hatarajii kusikia yeyote akidai kuwa hana au amechelewa kupata nakala hiyo, kwani waliondoka nazo katika mkutano uliotangulia.

Mkutano wa mwaka huu utakwenda vizuri na sitatarajii mjumbe yeyote kudai hajapata au amechelewa kutumiwa nakala hiyo ya rasimu ya Katiba wakati kila mmoja aliondoka nayo wakati wa mkutano uliopita, alisema Nyambui.

No comments:

Post a Comment