Sunday 1 March 2015

Mali mabingwa wapya Afrika U17



NIAMEY, Niger
MALI imetawazwa kuwa mabingwa wa Afrika kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 17 baada ya kuifunga Afrika Kusini kwa bao 2-0 katika fainali iliyofanyika jijini hapa.
Mabao ya kipindi cha pili yaliyowekwa kimiania na Siaka Bagayoko na Aly Malle yaliiwezesha Mali kutwaa taji hilo.
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Mali timu yake ya vijana inayojulikana kama Eaglets kushinda taji la mashindano ya vijana.
Awali, nchi hiyo ilikaribia kushinda taji mwaka 1997, wakati ilipomaliza ya pili nyuma ya washindi Botswana.

Timu zote Mali na Afrika Kusini zilienda katika fainali hiyo ya Jumapili zikiwa tayari zimewahi kukutana katika hatua ya makundi ya mashindano hayo, wakati Afrika Kusini ikiwa nyuma kwa bao 2-0 na kulazimisha sare ya 2-2.
Hatahivyo, Mali haikuruhusu hilo utokea tena, na kuhakikisha inaweka ulinzi mkali baada ya kupata bao la kuongoza na kuhakikisha inaibuka na ushindi.
Bao lao la kwanza lilipatikana baada ya dakika 67 wakati Bagayoko alipofunga kwa kichwa mpira wa kona.
The Eaglets waliongeza bao la pili zikiwa zimebaki dakika 12 kufuatia juhudi binafsi ya Aly Malle. Bao hilo alilifunga kutoka umbali wa kama mita 20 kutoka nje ya boksi na kuibua furaha kwa mashabiki wao.
Afrika Kusini walifikiri wangeweza kupata bao la kufutia machozi wakati Khanyisa Eric Mayo alipokaribia kufunga, lakini alijikuta akiwa ameotea.

No comments:

Post a Comment