Tuesday 31 March 2015

Wapinzani wachukua nchi Nigeria baada ya kumuangusha Jonathan


Rais Goodluck Jonathan (kushoto) na Muhammadu Buhari wiki iliyopita walikubaliana kukubali matokeo ya uchaguzi.

ABUJA, Nigeria
MTAWALA wazamani wa kijeshi Muhammadu Buhari amekuwa mgombea wa kwanza wa upinzani kushinda uchaguzi mkuu nchini Nigeria.

Chama cha Jenerali Buhari kilisema kuwa, mpinzani wake ambaye alikuwa rais wa Nigeria Goodluck Jonathan, alikubali matokeo hayo na kumpongeza mwanajeshi huyo mstaafu.

Wakati akikubali kushindwa, Jonathan alikuwa amepitwa na Buhari karibu kura milioni mbili.

Waangalizi wa uchaguzi huo waliupongeza lakini kulikuwa na tetesi za vurugu, zilizosababisha wasiwasi kuwa zingesababisha maandamano na vurugu.

"Rais Jonathan alimpigia simu Jenerali Muhammadu Buhari, mshindi wa uchaguzi, kumpngeza, alisema Lai Mohammed, ambaye ni msemaji wa Chama cha Jenerali cha All Progressives Congress (APC).

Msemaji alimpongeza Bwana Jonathan, akisema: "Atabaki kuwa shujaa wan chi hii kwa kitendo chake cha kukubali matokeo."

"Yeyote atakayejaribu kuleta vurugu kwa madai ya kushindwa katika uchaguzi atakuwa akifanya hilo kwa faida yake, " aliongeza.

Hiki ni kipindi muhimu kwa historia ya Nigeria. Haijawahi kutokea rais aliye madarakani kushindwa katika uchaguzi.

No comments:

Post a Comment