Saturday 28 March 2015

Wanafunzi Filbert Bayi watesa mbio za nyika Zanzibar




Wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari ya Filbert Bayi wakiwa nje ya hosteli ya Magereza (Chuo cha Mafunzo) Zanzibar katika picha ya pamoja na viongozi wa timu hiyo iliyoshiriki mbio za nyika mjini Zanzibar. Kushoto mstari wa nyuma ni kocha wa timu hiyo Zacharia Gwandu. Kulia nyuma ni matroni `Mama Mdogo.

Baadhi ya washiriki wa mbio za nyika za kilometa nne za wanafunzi wasichana wakijiandaa kushiriki mbio hizo Jumamosi.

Baadhi ya wanafunzi kutoka shule za pembezoni mwa kisiwa cha unguja wakiwasili kwenye uwanja wa Maisala kwa ajili ya kushiriki mbio za nyika za Zanzibar Jumamosi.

Kocha wa timu ya riadha ya shule za Filbert Bayi Zacharia Gwandu akiwapa maelekezo wachezaji wake kabla hawajashindana katika mbio za nyika Zanzibar Jumamosi.
Wanafunzi wa shule ya Filbert Bayi wakipozi kwa picha katika bahari mjini Zanzibar ambako walikwenda kushiriki mbio za nyika za shule za msingi na 
sekondari ambazo zilitakiwa na shule hiyo ya Mkuza Kibaha mkoani Pwani.

Baadhi ya washiriki wa mbio za nyika za kilometa nne za wanafunzi wasichana wakijiandaa kushiriki mbio hizo Jumamosi.


Upendo! Dorcus Boniface (kushoto) akionesha upendo kwa kumpatia maji mwanariadha mwenzake wa shule ya Filbert Bayi Jumamosi.

                         
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Ali Juma Shamhuna akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa Filbert Bayi wakati wa mashindano ya mbio za nyika .
Washiriki wa shule ya  Filbert Bayi kabla ya kuanza mbio.
Baadhi ya washiriki wakiwa wamejipanga kabla ya kuanza mbio hizo Jumamosi mjini Zanzibar.

Baadhi ya washiriki wa mbio za kilometa nne kwa wasichana wa shule za msingi wakielekea sehemu ya kuanzia mbio za Nyika katika viwanja vya Maisala Jumamosi.


One Two three, One Two Three! Wanafunzi wa shule ya Filber Bayi wakiongoza katika mbio za kilometa nne kwa wasichana wa shule ya msingi. Wanafunzi hao ndio walishika nafasi tatu za kwanza.


Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Filbert Bayi wakiwaongoza washiriki wengine wa mbio za nyika za kilometa sita wakati wakielekea kuanza mbio hizo Jumamosi mjini Zanzibra. Timu hiyo ndio ilishinda.
 

No comments:

Post a Comment