Tuesday 3 March 2015

Rais Kenyatta atechoma pembe za tembo za mabilioni




NAIROBI, Kenya
RAIS wa Kenya Uhuru Kenyatta amechoma moto tani 15 za pembe za ndovu ikiwa ni sehemu ya juhudi za mataifa ya Afrika Mashariki kupiga vita uwindaji haramu.
Pembe hizo za ndovu katika soko la mitaani inafikia thamani ya kiasi cha dola za Marekani Milioni 30 (sawa na pauni Milioni 19.4), ikiwa ni kiasi kikubwa kuharibiwa nchini Kenya.

"Pembe hizi nyingi ni mali ya tembo ambao waliuawa na majangiri," alisema katika hafla hiyo ya kuchoma moto pembe hizo katika mbuga za hifadhi ya taifa.
Pembe za ndovu zimekuwa na soko kubwa huko Asia kwa ajili ya mapambo.
Katika soko la mitaani, kilo moja ya pembe ya ndovu ina thamani ya dola za Marekani 2,000.
Faru nao wanawindwa kwa ajili ya pembe zao kwa ajili ya dawa za asili.
Watu wa mazingira wameonya kuwa tembo watatoweka kabisa katika baadhi ya nchi za Afrika katika kipindi cha miaka michache ijayo.
"Miaka 25 iliyopita baada ya historia ya kuchoma pembe za ndovu, mahitaji ya soko kwa mara nyingine tena yamekuwa tishio kwa tembo wa Afrika na faru, " alisema Rais Kenyatta.

No comments:

Post a Comment