Tuesday 25 August 2015

Dk. Ali Mohamed Shein awahutubia maelfu ya wananchi Zanzibar

Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein akiwahutubia wanachama wa CCM na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Kibandamaiti mjini Zanzibar jana. Shein alichukua fomu kutaka kuwania tena nafasi hiyo.

Polisi yampiga stop Lowassa kutembelea wananchi uswahilini



Waandishi Wetu
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limemuonya mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa, kuwa staili ya kampeni aliyoianzisha ya kutembelea maeneo mbalimbali katika ziara zisizo rasmi, inahatarisha usalama wa raia na mali zao, hivyo iachwe.

Onyo hilo limewagusa pia wagombea wa vyama vya siasa katika nafasi mbalimbali hasa urais, ikielezwa kuwa, katika ziara hizo hujitokeza watu wengi, ambapo pia wahalifu wanaweza kutumia mwanya huo kufanya vitendo vya uhalifu.

Akizungumza na vyombo vya habari jana jijini Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi wa kanda hiyo, Suleiman Kova alisema, baadhi ya wagombea wa vyama vya siasa wameanzisha mtindo wa kutembelea maeneo mbalimbali kama vituo vya daladala na masoko kwa madai ya kuyatembelea makundi ya watu wenye kipato cha chini.

Kamishna Kova alisema, kutokana na uzoefu uliojitokeza katika ziara hizo zisizo rasmi, imeonekana mikusanyiko mikubwa isiyotegemewa katika hali inayoashiria uvunjifu wa amani.

Kova alisema lengo la marufuku hiyo haliko kisiasa bali ni kwa ajili ya usalama wa wananchi wote, kwani wao wanafanya kazi kwa mujibu wa sheria na si siasa.

Alitaja miongoni mwa wagombea hao ni mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chadema, Edward Lowassa pamoja na mgombea mwenza, Juma Duni Haji, ambaye jana alikuwa akifanya ziara yake katika eneo la Kariakoo, wilaya ya Ilala.

Alisema saa 6:00 mchana katika makutano ya mtaa wa Swahili na Uhuru, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Lucas Mkondya alilazimika kukutana ana kwa ana na Lowassa ili kumpa tahadhari ya kiusalama.

Mgombea huyo alikuwa amezungukwa na wapanda pikipiki wasiopungua 40 pamoja na magari mengi, hali ambayo ilileta msongamano katika eneo hilo.

Lazima ieleweke wazi kwamba moja ya kazi za Jeshi la Polisi ni kudhibiti makundi makubwa ya watu katika namna ambayo kiongozi yeyote wa aina ya wagombea urais anatakiwa kulindwa katika kipindi chote cha kampeni hadi siku ya uchaguzi, alisema Kova.
Alisema ni vyema wagombea mbalimbali hasa wa urais waoneshe ushirikiano wa hali ya juu kwa Jeshi la Polisi ili kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza dhidi yao au kwa watu wengine.

Alisema jambo hilo linaweza kuonekana ni kawaida lakini yakitokea madhara lawama zote zitaenda kwa polisi kwa kushindwa kufanya kazi yao.

Hata hivyo, alisema marufuku hiyo ni kwa vyama vyote vyenye wagombea wanaoshiriki katika uchaguzi mkuu na kwamba atakayeamua kukaidi agizo hilo atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Aidha, Kamanda Kova alishauri viongozi wa vyama pamoja na wagombea wao kufuata ratiba za kampeni za mgombea urais na mgombea mwenza kwa vyama vya siasa kama ilivyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ili kuondoa hisia za kufanyika kampeni nje ya ratiba.

DEATH ANNOUNCEMENT



The late Eng. Lambert Ndiwaita

The Ministerial Advisory Board (MAB), Management and Staff of Tanzania Airports Authority (TAA) regret to announce the untimely death of the TAA Board Chairman, Eng. Lambert W. Ndiwaita who passed away at Nairobi Hospital, Kenya on 20th August, 2015. He will be buried at his home village in Bukoba on 25th August, 2015.

Eng. Lambert Ndiwaita (64) was one the prominent aviation experts who contributed significantly in the development of aviation industry. He started his carrier in 1971 when he joined the then Ministry of Works as an Assistant Executive Engineer and later rose to the position of Chief Engineer for Roads and Aerodromes. In 1993, he worked as an expatriate with the Department of Civil Aviation in Botswana where he assisted in the establishment of an Aerodrome Maintenance section. Later, in 1994 he joined the International Civil Aviation Organization (ICAO) as Technical Officer (later Regional Officer) for Aerodromes & Ground Aids (AGA) at the ICAO's, Eastern & Southern Africa Regional Office in Nairobi, Kenya until his retirement in 2014 . While at ICAO regional office, his main duties were to insure uniform implementation of ICAO Standards and recommended practice in the fields of Aerodromes and Ground Aids in 23 States accredited to the ESAF Regional Office. He was also responsible for the uniform implementation of the International Civil Aviation Security Standards and for coordinating technical cooperation activities to assist States with difficulties in standards implementation.

Eng. Lambert Ndiwaita pursued his Civil Engineering undergraduate training at the University of Nairobi where he obtained his Bachelor of Science. In 1978, he pursued Postgraduate studies of Master of Science in Civil Engineering at the University of California, Berkley, USA where he specialized in Aerodrome Engineering & Maintenance after which he returned to serve in the then Ministry of Works'; Roads & Aerodromes Department.

He will be remembered for his dedication and expertise in the development of aviation sector especially in upgrading and expansion of Mwanza, Tabora, Kigoma, Songwe, Mafia, Mpanda, Bukoba and Julius Nyerere International Airport (JNIA).

May the Almighty God Rest his Soul In Peace. Amen.

ISSUED BY THE OFFICE OF THE DIRECTOR GENERAL
TANZANIA AIRPORT AUTHORITY
24th AUGUST, 2015

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Afariki Dunia, kuzikwa leo kwao Bukoba Mjini



MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE TANZANIA


TANGAZO LA KIFO



         Hayati Mhandisi Lambert W. Ndiwaita


Bodi  ya Ushauri, Menejimenti na Wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) wanasikitika  kutangaza kifo cha  Mwenyekiti wa Bodi  ya TAA,   Inj. Lambert W. Ndiwaita  kilichoteka  tarehe 20/08/2015  katika  Hospitali  ya Nairobi,  Kenya.  Marehemu anatarajiwa kuzikwa nyumbani kwake mjini Bukoba  tarehe 25/08/2015.

Mhandisi  Lambert Ndiwaita (64)  ni mmoja wa wataalamu waliobobea katika masuala ya  usafiri wa anga  kitaifa na kimataifa, katika kipindi cha uhai wake ametoa mchango mkubwa katika  maendeleo ya sekta hiyo hapa nchini na nchi  nyingine duniadi.

Alianza shughuli zinazohusiana na  usafiri wa anga mwaka 19971  alipoajiriwa na iliyokuwa  Wizara ya  Ujenzi  kama  Mhandisi  Msaidizi na baadaye alipanda hadi   kufikia cheo cha  Mhandisi Mkuu  (Chief Engineer) akishughulikia masuala ya baeabara na  viwanja vya ndege. Mwaka 1993 alikwenda kufanya kazi katika Idara ya Usafiri wa Anga nchini Botswana kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Mwaka 1994 aliajiriwa na  Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga  International Civil Aviation Organization (ICAO)  kusimamia  masuala ya  viwanja vya ndege (Aerodrome & Ground Aids) kwa eneo  la Mshariki na kusini mwa Afrika, katika ofisi za ICAO  zilizopo jijini Nairobi, Kenya.

Mhandisi Ndiwaita ni msomi aliyehitimu Shahada ya kwanza ya Uhandisi (Bsc Civil Engineering) katika Chuo Kikuu cha Nairobi. Mwaka 1978 alihitimu  masomo Shahada ya Uzamili (Msc in Civil Engineering) katika Chuo kikuu cha Califonia, Berkley, nchini Marekani akijitikita zaidi katika masuala uhandisi wa ujenzi wa viwanja vya ndege.

Marehemu Lambert Ndiwaita atakumbukwa  na  wadau wa usafiri wa anga nchini na duniani kwa  mchango  mkubwa katika  maendeleo ya sekta hiyo  ambapo  kwa hapa nchini akiwa  Mwenyekiti wa Bodi  ya TAA  amechangia   kufanikisha ujenzi na uboreshaji wa viwanja  kadhaa  vikiwemo Mwanza, Tabora, Kigoma, Songwe,Mafia, Mpanda, Bukoba na Julius Nyerere  (JNIA).

Mungu ailaze roho marehemu  mahala pema peponi.

Imetolewa na Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu-TAA.
24th AUGUST, 2015
Agosti 12, 2015