LONDON, England
HAKUNA timu, katika mfumo wa sasa wa mashindano,
iliyowahi kusonga mbele ikihitaji zaidi ya bao moja la ugenini, ambapo the
Gunners wanaangalia kubadilisha matokeo ya kufungwa 3-1 katika mchezo wa
kwanza.
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amewataka wachezaji
wake kuamini kuwa wanaweza kubadili matokeo hayo wakati kesho Jumanne
watakapokutana na Monaco katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.
Klabu hiyo ya Ligi Kuu ya England ilipokea kichapo cha
3-1 wakati timu hizo zilipokutama katika mchezo wa kwanza wa mechi za timu 16
bora kwenye uwanja wa Emirates mwezi uliopita.
Hakuna timu katika kipindi cha Ligi ya Mabingwa wa
Ulaya imewahi kusonga mbele wakati ikihitaji ushindi wa zaidi ya bao moja ugenini ili kukwepa kuondolewa
katika mashindano hayo.
Endapo itashindwa kubadili matokeo hayo, basi Arsenal
itakuwa imeondolewa kwa msimu wa tano mfululizo katika hatua ya kwanza.
Ratiba
Ligi ya Mabingwa Ulaya Jumanne Machi 17,2015:
Atlético de Madrid
v Bayer 04 Leverkusen Saa 4:45 usiku.
Monaco v Arsenal Saa
4:45 Usiku.
Jumatano
Machi 18, 2015:
Borussia Dortmund v Juventus saa
4:45 usiku.
Barcelona v Manchester City saa 4:45 usiku.
No comments:
Post a Comment