Tuesday 3 March 2015

MDOMO WAMPONZA CARLTON COLE



LONDON, England
MSHAMBULIAJI wa West Ham Carlton Cole ameshitakiwa na Chama cha soka cha England kwa maoni yake aliyoyatoa katika mtandao wa kijamii.
Shitaka hilo linahusiano na kile alichoweka katika mtandao huo wa kijamii mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 kuhusu shabiki wa Tottenham kufuatia sae ya kufungana bao 2-2 kati ya timu hizo februaria 22 katika mchezo wa Ligi kuu ya England.
Taarifa ya Chama cha Soka ilisema: "Inadaiwa kuwa maoni yake yalikuwa yaudharirishaji na kuumiza na kuuweka mchezo wa soka matatani.
Cole mbaye ni mshambuliaji wazamani wa timu ya taifa ya England amepewa hadi machi 5 awe amejibu mashtaka hayo.
Cole ameichezea The Hammers mechi 17 msimu huu na kufung mabao matatu.
Alipigwa faini na Chama cha Soka kutokana na maoni yake aliyoyatoa katika Twitter wakati wa mchezo wa kirafiki wa kimataifa wa England na Ghana Aprili mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment