Thursday 5 March 2015

Rudisha kukimbia IAAF Diamond League


Mwanariadha wa Kenya David Rudisha.

NAIROBI, Kenya
BINGWA wa Olimpiki na anayeshikilia rekodi ya dunia David Rudisha amethibitisha kushiriki katika mbio za IAAF Diamond League itakayofanyika Juni 7 mwaka huu.

Mbio hizo za aina yake zinatarajia kufanyika Sainsbury huko Birmingham.

Rudisha alifanya kweli wakati wa Michezo ya Olimpiki iliyofanyika London mwaka 2012 wakati aliposhinda mbio za mita 800 akiongoza kuanzia mwanzo wa mbio hadi mwisho.

Mwanariadha huyo wa Kenya alishinda mbio hizo kwa kutumia dakika 1:40.91, ambapo Mkenya huyo anataka kuonesha makali yake atakaporejea tena katika ardhi ya Uingereza mwezi Juni.

“Napenda sana kushiriki mbio Uingereza na sitasubiri kujipanga katika mbio za Sainsbury's Birmingham Grand Prix, alisema.

“Nina kumbukumbu nzuri ya kushinda zaidi ya mita 600 huko Birmingham katika kipindi kilichopita cha majira ya joto nilipoweka rekodi ya dunia katika Olimpiki ya London 2012.

Nategemea naweza kurudia kiwango kile nilichokuwa nacho wakati ule…”

Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 26 mara pekee kwa mara ya mwisho alishinda Birmingham mwaka jana katika mashindano kama hayo, ambako alishinda mbio za mita 600.

Rudisha alishinda taji la dunia mwaka 2011 na anatarajia mbio hizo za  Birmingham Grand Prix zitakuwa muhimu kabla hajajaribu kutwaa tena taji hilo Beijing mwezi Agosti.

No comments:

Post a Comment