Sunday 15 March 2015

Tigo yazindua mnara mpya wa kisasa kijijini Iringa





*kupanua upatikanaji wa huduma za mawasiliano mikoa ya kusini


TIGO Tanzania imezindua mnara mpya katika kijiji cha Magubike mkoani Iringa jambo linakusudia kutoa fursa mpya za kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa eneo hilo.

Kutokana na maelezo ya Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo Bi. Cecile Tiano, mnara huo mpya ni kati ya minara 843 iliyopangwa kujengwa nchini kote mwaka huu,  ambapo minara 348 au asilimia 41 ya minara yote itajengwa katika mikoa ya nyanda za juu kusini ikiwemo Iringa, Ruvuma, Njombe, Mbeya na Rukwa.

Mnara huu wa Magubike umejengwa kwa ushirikiano na serikali kupitia mpango maalum wa kufikisha mawasiliano nchini kote uitwao Universal Communication Services Access Fund (UCSAF). Mpango ambao unategemea kuchagiza maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika maeneo ya vijijini na mijini kupitia mfumo wa TEHAMA na ambao utahakikisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo ya vijijini na mijini. 

Akizindua mnara huu mpya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Juma Masenza, alikaribisha uwekezaji wa kampuni hiyo akisisitizia kwamba mnara huo utasaidia kufungua fursa za kijamii na kiuchumi zilizopo katika mkoa huo. 

Masenza alisema, Napenda kuchukua fursa hii kuwahakikishia wawekezaji katika sekta ya mawasiliano kwamba serikali itaendelea kushirikiana nao na wadau wengine wa maendeleo kwa kuwapatia mazingira bora ya kufanyia biashara kwa ajili ya kuboresha sekta ya mawasiliano nchini.

Wakati huohuo; Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo Bi. Cecile Tiano alisema kampuni hiyo imekuwa ikiwekeza wastani ya dola za kimarekani milioni mbili kwa wiki katika upanuzi wa mtandao na uboreshwaji wa huduma zake nchini kote ndani ya miaka miwili iliyopita ikiwa na lengo la kuwezesha watu kuishi maisha ya kidijitali.

Akielezea kuhusu umuhimu wa huduma za mawasiliano kwa wakazi wa eneo hilo, Meneja Mkuu huyo alisema kwamba Tigo Kilimo, ni huduma mojawapoo watakayofaidika nayo.  huduma nayowasaidia wakulima kupata habari muhimu kama vile bei za mazao, utabiri  wa hali ya hewa na taarifa tofauti tofauti za kilimo kupitia simu zao. Pia watu wanaweza kufaidika kiuchumi kwa kuwa wakala wa Tigo Pesa.

Alisema Tigo pia ina mipango ya kuongeza matawi yake ya huduma kwa wateja katika mikoa hiyo mitano, kutoa fursa za vijana kujiajiri kupitia kuwa wakala wa kujitegemea wa Tigo pamoja na kuchangia miradi mbalimbali ya kijamii kupitia mpango wake wa uwajibikaji kwa jamii.

Kuhusu Tigo:
Tigo Tanzania ni kampuni ya mawasiliano inayoongoza kwa ubunifu nchini, inafahamika kama kampuni inayolenga kuleta maisha ya kidijitali katika jamii. Inatoa huduma tofauti tofauti za mawaliano kwa njia ya simu, intanet ya kasi na kutuma na kupokea fedha. Aidha Tigo imebuni bidhaa na huduma mbali mbali kama Facebook kwa Kiswahili, Tigo Pesa App kwa watumiaji wa simu za Android na iOS, na ni kampuni ya simu ya kwanza Afrika Mashariki kuanzisha huduma ya kutuma na kupokea pesa kwa njia ya simu kimataifa, yenye uwezo wa kubadilisha fedha za kigeni.
Kwa kutumia tekinolojia ya 3G Tigo ina wahakikisha wateja upatikanaji wa huduma bora na za uhakika. Kati ya mwaka 2013 na 2014, kampuni ilizindua minara mipya zaidi ya 500 na pia ina mipango wa kuongeza mara mbili kiwango cha uwekezaji ifikapo mwaka 2017 ili kuweza kupanua wigo wa mawasiliano na uwezo wa mtandao hasa hasa katika maeneo ya vijijini. Tigo ina wateja zaidi ya milioni 8 na inatoa ajira za moja kwa moja na kwa namna mbali mbali kwa Watanzania zaidi ya 100,000 ambao wanajumuisha wafanyakazi wa huduma kwa wateja, wa kutuma na kupokea fedha, watu wa mauzo pamoja na wasambazaji.
Tigo ni kampuni ya simu inayoongoza chini ya kampuni mama ya mawasiliano Millicom, ambayo imejizatiti katika kuhamasisha na kufanikisha maisha ya kidijitali katika nchi 44 zenye biashara zake Afrika na Latin Amerika, pamoja na ofisi za kampuni zilizopo Ulaya na Marekani. Kwa kutambua kwamba ubunifu ndio utakaowafanya kuendelea kuwa juu ya ushindani, Millicom inaendelea kuthamini mchango wa wadau wake, wakitumia dhana ya demand more kama namna ya kufanya biashara na kuendeleza nafasi yao kama kampuni inayoongoza katika kufanikisha maisha ya kidijitali katika baadhi ya masoko makubwa yenye ushindani mkali duniani.
TABASAMU, UKO NA TIGO
Kwa maelezo zaidi tembelea:  www.tigo.co.tz au wasiliana na:
John Wanyancha Meneja Mawasiliano
Simu: 0658 123 089

Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo, Cecile Tiano (mwenye miwani) pamoja na Mkurugenzi wa Tigo Nyanda za Juu Kusini, Jackson Kiswaga (nyuma yake) wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Magubike wakati kampuni hiyo ilipokuwa ikizindua mnara wake wa mawasiliano katika kijiji cha Magubike, Iringa Vijijini.

Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo, Cecile Tiano (mwenye miwani) pamoja na Mkurugenzi wa Tigo Nyanda za Juu Kusini, Jackson Kiswaga wakifuatilia jambo wakati kampuni hiyo ilipokuwa  ikizindua mnara wake wa mawasiliano katika kijiji cha Magubike, Iringa Vijijini.
Mrajisi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Iringa, John Kiteve kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza akisoma hotuba ya kuishukuru kampuni ya mawasilino ya Tigo baada ya kujenga na kuzindua mnara wake wa mawasiliano katika kijiji cha Magubike, Iringa vijijini.
Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo, Cecile Tiano (mwenye miwani) na Mrajisi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Iringa, John Kiteve (wa pili kulia) wakikata utepe kwa pamoja kuzindua rasmi mnara wa kisasa wa mawasiliano katika kijiji cha Maagubike, Iringa Vijijini.
Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo, Cecile Tiano (mwenye miwani) pamoja na viongozi wengine wa Tigo, halmashauri ya Iringa na mkoa wa Iringa wakiwa katika picha ya pamoja na timu soka ya kijiji cha Ilalasimba iliyocheza na timu ya kijiji cha Magubike baada ya uzinduzi wa mnara wa kisasa wa mawasiliano wa Tigo katika kijiji cha Magubike, IringaVijijini.

Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo, Cecile Tiano (mwenye miwani) pamoja na viongozi wengine wa Tigo, halmashauri ya Iringa na mkoa wa Iringa wakiwa katika picha ya pamoja na timu soka ya kijiji cha Magubuke iliyocheza na timu ya kijiji cha Ilalasimba baada ya uzinduzi wa mnara wa kisasa wa mawasiliano wa Tigo katika kijiji cha Magubike, IringaVijijini

Mrajisi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Iringa, John Kiteve kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza akisoma hotuba ya kuishukuru kampuni ya mawasilino ya Tigo baada ya kujenga na kuzindua mnara wake wa mawasiliano katika kijiji cha Magubike, Iringa vijijini.
Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo, Cecile Tiano (katikati) akisoma hotuba yake mara baada ya kampuni hiyo ya mawasiliano kuzindua mnara wake wa masiliano katika kijiji cha Maagubike, Iringa Vijijini.

No comments:

Post a Comment