MADRID, Hispania
KOCHA Carlo Ancelotti
(pichani) anasema kuwa kamwe hatabadilisha "sura" wa kikosi chake cha Real
Madrid, licha ya washambuliaji wake kuwa butu.
Karim Benzema,
Cristiano Ronaldo na Gareth Bale walipambana dakika za mwisho, huku Real Madrid
ikishindwa kufunga katika mechi mbili zilizopita.
WBale aliyesainiwa
kwa rekodi ya dunia hajafunga katika mechi zake nane zilizopita, lakini
anatetewa na kocha wake.
"Wamefunga
machache katika mecgi zilizopita lakini nafikiri tunatakiwa kuwasaidia
washambuliaji, " alisema Ancelotti.
"Hatutabadili
sura ya timu yetu kwa sababu hilo ndilo linatufanya tujisikie vizuri zaidi, "
aliongezakocha huyo Muitalia. "Bila wasiwasi wowote nina imani nao.
"Nitamuacha Karim
kwa sababu hajafunga katika mechi chache. Nimuache Cristiano. Sifikiri kama
Bale atakuwa na furaha kwa jinsi anavyocheza lakini najua kuwa anatakiwa
kuimarisha zaidi."
Bale ambaye ni
mchezaji wazamani wa Tottenham na mchezaji mwenzake Luka Modric alirejea katika
kikosi cha Real kwa mara ya kwanza tangu alipoumia misuli Novemba huku klabu
yake ya Hispania ikiongoza kwa jumla ya mabao 2-0 huko Gelsenkirchen katika
mchezo wa kwanza.
No comments:
Post a Comment