Tuesday 3 March 2015

KIPA IVORY COAST ASTAAFU SOKA LA KIMATAIFA




ABIDJAN, Ivory Coast
KIPA wa timu ya taifa ya Ivory Coast au Tembo kama inavyojuliana sana Boubacar Barry ametangaza kustaafu soka la kimataifa, chini ya mwezi mmoja baada ya kuiwezesha nchi hiyo kutwaa taji la Mataifa ya Afrika.
Barry, 35, alifanya kazi kubwa katika fainali wakati tembo hao wakiwachapa Ghana kwa penati na kutwaa taji hilo Februaria 8 mwaka huu.
Kipa huyo aliokoa penati mbili wakati wakupigiana penati kabla hajafanya kazi ya ziada kufunga ya ushindi iiyowapatia taji Ivory Coast.
"Vitu vyote vizuri lazima viwe na mwisho. Nimeamua kumaliza kipindi change ca kuichezea Ivory Coast. Nilikuwa najiunia kuvaa jezi ya nchi yangu, " alisema Barry katika ukurasa wake wa Facebook.
Barry ameichezea Iory Coast mechi 86 na kushiriki katika fainali za Kombe la Dunia mara taty, yaani 2006, 2010 na 2014.
Pia kipa huyo alikuwa langoni mwaka 2012 wakati wa fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika ambako Ivory Coast ilifungwa na Zambia kwa penati.

No comments:

Post a Comment