Wednesday 11 March 2015

Tigo watoa msaada wa Milioni 30 kwa waathirika wa mafuriko Kahama








TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tigo yatoa msaada wa millioni 30 Tshs kwa waathirika wa mafuriko mjini Kahama

Tigo imetoa msaada wa vyakula na vifaa vya kutumika nyumbani vyenye thamani ya millioni 30 kwa familia zilizoathirika na mvua kubwa ya mawe na mafuriko wiki iliyopita, iliyosababisha vifo vya watu zaidi ya 50 mjini Kahama, mkoani Shinyanga

Vifaa hivyo vilikabidhiwa leo kwa waathirika wa mafuriko na Mkurugenzi wa Tigo kanda ya ziwa Bwana Ally Maswanya, alie sisitiza ahadi ya kampuni kusimama kidete na wananchi katika wakati wa faraja na shida.

 “Tupo hapa kujumuika na wasamaria wema wengine katika kuwapa pole walioathirika na maafa hayo, na tunawaombea kila la kheri waweze kurudi katika hali tulivu baada ya kupoteza wapenzi wao na mali zao,” Alisema Maswanya.

Vifaa vilivyo tolewa na Tigo ni magodoro, unga wa mahindi,mchele,maharage,dagaa,mafuta ya kula,chumvi,sukari,ndoo,sabuni, karai, vikombe na masahani.

Tigo pia kwa kupitia mtandao wake, imejitolea kuchangisha kwa ajili ya kusaidia waathirika wa mafuriko, ambapo mteja wa Tigo anaweza kutuma ujumbe mfupi kwenda namba 15741 kwa ajili ya kuchangia Tshs 200 kutoka kwa mda wake wa maongezi au kupitia vipochi vyao vya Tigo Pesa kuenda namba 0714048435.

Mvua zilizonyesha mjini Kahama, wiki iliyopita, iliripotiwa kwamba zilisababisha vifo vya watu zaidi ya 50 na kuacha watu 3,500 kukosa sehemu za kulala, na pia mimea na makazi ya watu yaliharibika au kubebwa na mafuriko, taarifa hii ni kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga.

Msaada kutoka Tigo, kulingana na Maswanya, ni katika mpango wake wa uwajibikaji kwa jamii, sera hii ni ahadi kwa ajili ya kuwekeza baadhi ya rasilimali za kampuni katika miradi ya kuendeleza na pia katika kusaidia jamii majanga yanapo ibuka.
Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa, Bw.Ally Maswanya(kulia) akimkabidhi baadhi ya vyakula, vilivyio gharimu milioni 30 ,Mkuu wa wilaya ya Kihama Bw.Benson Mpesya(kushoto) kwa ajili ya waathirika wa mafuriko,  katika kijiji cha Mwakata, wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Baadhi ya magodoro na vyakula vilivyotolewa na Tigo, kama msaada kwa waathirika wa mafuriko katika kijiji cha Mwakata, wilaya ya Kahama,mkoani Shinyanga.
Wanakijiji wa Mwakata walioathirika na mafuriko, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Bw. Ally Maswanya(hayupo pichani), baada ya kutoa msaada wa vyakula na vifaa vya ndani ya nyumba vilivo gharimu Sh.Milioni 30.

 

No comments:

Post a Comment