Na Seba Nyanga
MABONDIA Kalama Nyilawila na Mada Maugo watapanda ulingoni Machi
Jumapili Machi 15 katika Uwanja wa Taifa wa Ndani kutwangana katika pambano na
ndondi za kulipwa.
Pambano hilo limeandaliwa na Mwazoa Promotion na viingilio
vitakuwa Sh. 10,000 kwa eneo la kawaida na Sh. 20,000 kwa wale watakaokaa
katika viti maalum (VIP).
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa hivi karibuni jijini Dar es
Salaam, kutakuwa na mapambano kadhaa ya utangulizi ili kunogesha pambano hilo
linalosubiriwa kwa hamu.
Katika pambano la kwanza la utangulizi, Abdallah Pazi atazichapa
na Thomas Mashali katika pambano la raundi 10 wakati Said Mbelwa atakuwa na
kibarua kizito wakati atakapotoana jasho na Japhet Kaseba.
Mbali na hayo, pia kutakuwa na mapambano mengine ya utangulizi
ambayo yatatangazwa siku hiyo ya mpambano ili kutoa burudani zaidi kwa wapenzi
watakaofika Uwanja wa Taifa wa Ndani siku hiyo.
Waandaji wamesema kuwa siku hiyo pia kutauzwa DVD za mapambano
mbalimbali makali pamoja na vifaa vingine ambavyo vitauzwa na kocha mahiri wa
ndondi Super D.
No comments:
Post a Comment