Mheshimiwa Mgeni Rasmi, Ndugu Semu Mwakanjala,
Kaimu Meneja Mawasiliano kwa Umma, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA),
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Meja Mstaafu
Ndugu Filbert Bayi,
Viongozi wa Elimu Mkoa wa Pwani,
Wajumbe wa Bodi za Shule,
Wazazi, Wafanyakazi, Wanafunzi,
Wageni waalikwa, Mabibi na Mabwana.
Tunamshukuru Mungu kwa upendo na rehema tele kutuwezesha
kukutana tena mwaka huu 2015, kwenye mahafali ya watoto wetu wa darasa la saba
na kidato cha nne.
Ninawashukuru kipekee wazazi, na wageni wote
mliokubali mwaliko wetu na kuhudhuria sherehe ya leo ya:-
-
Mahafali ya 5 ya shule ya msingi Kibaha yenye
wahitimu 21
-
Mahafali ya 14 shule ya Msingi Kimara yenye
wahitimu 47
-
Mahafali ya 10 shule ya Sekondari yenye
wahitimu 83
HISTORIA YA SHULE YA CHEKECHEA NA MSINGI
Mhe. Mgeni rasmi shule zetu za
chekechea na msingi ziko katika makundi mawili kama ifuatavyo:-
i)
Kimara Dar es Salaam
Mwaka 1996 tulianzisha shule ya
chekechea na msingi iliyopo Kimara na tulipata usajili mwaka 2000 kwa namba
DS/02/7/007. Mpaka sasa shule ina jumla
ya wanafunzi 584 pia tunao waalimu 40 na wafanyakazi wasio waalimu 31.
ii) Mkuza
– Kibaha
Shule
hii ilisajiliwa mwaka 2010 kwa namba PW.01/7/008. Na ina jumla ya wanafunzi 339, waalimu 17 na wafanyakazi wasio waalimu 10.
HISTORIA YA SHULE YA SEKONDARI
Mhe. Mgeni Rasmi Shule ya Sekondari Filbert Bayi
ilianzishwa rasmi mwaka 2003 kule Kimara palipo na shule ya Msingi na hatimaye
majengo yalipokamilika Februari, 2004 tulihamia huku Kibaha na tarehe 2 / 3
/2005 kuzinduliwa rasmi na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
awamu ya tatu Mhe. Benjamin William Mkapa.
Shule imesajiliwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kupitia namba ya
usajili S.1377 na kituo cha mtihani namba S.1437.
MAFANIKIO NA MAENDELEO YA SHULE
Mhe.
Mgeni Rasmi shule zetu zimepata mafanikio makubwa kitaaluma na michezo tangu
zilipoanzishwa kama ifuatavyo:-
i) Matokeo
ya Mitihani upande wa Msingi
-
Mwaka
2014 shule za msingi Kimara na Kibaha waliomaliza darasa la saba walifaulu kwa
asilimia mia moja (100%) na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwenye
shule za serikali, japo wengi wao walirudi Filbert Bayi.
ii) Matokeo
ya Mitihani upande wa Sekondari
Mwaka 2014 wanafunzi
38 walifanya mtihani wa kidato cha nne na matokeo yao ni kama ifuatavyo:-
·
Daraja la 1 - 6
·
Daraja la 2 - 11
·
Daraja la 3 - 18
·
Daraja la 4 - 3
·
Daraja la 0 - Hakuna
Tuna matarajio makubwa kwamba mwaka huu hawa wanafunzi wanaohitimu leo
watafanya vizuri zaidi na hii ni kutokana na juhudi na mikakati kabambe
waliojipangia Waalimu na wanafunzi.
ELIMU YA UJASILIAMARI
Pamoja na masomo ya darasani, vijana wetu wameanza kujifunza masomo ya
ujasiliamali kama ufugaji wa kuku, upambaji wa kumbi kwa ajili ya sherehe
mbalimbali, upishi, ususi, unyoaji, upambaji wa maharusi na utengenezaji
nywele.
Taaluma hizi ninaamini zitawasaidia kuwa wajasiliamali wakati wakisubiri
matokeo yao wamalizapo shule na vyuo.
Mhe. Mgeni Rasmi ni matumaini yangu kwamba utakuwa umepata kwa kifupi
mafanikio na maendeleo ya shule zetu.
HITIMISHO
Mhe.Mgeni Rasmi ili kukamilisha sherehe hii siku ya leo tutakuomba
ukabidhi vyeti na zawadi kwa wahitimu wote na zawadi maalumu kwa waliofanya
vizuri ikiwa ni pamoja na Kitaaluma, Uongozi bora, Nidhamu na Michezo.
ASANTENI KWA KUNISIKILIZA
No comments:
Post a Comment