Sunday 26 November 2017

Hotuba ya Mkurugenzi wa Shule za Filbert Bayi, Anna Bayi Siku ya Wazazi na Mahafali ya Chekechea 2017



Ndugu Akofa Ata, Mkurugenzi Mkazi, Unilever Tanzania

Ndugu Meja Mstaafu Filbert Bayi M/kiti, Bodi ya Wakurugenzi,
Viongozi wa Elimu Mkoa wa Pwani,
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi,
Wajumbe wa Bodi ya Shule,
Wanakamati wa shule, Wazazi,
Wafanyakazi, Wanafunzi,
Wageni waalikwa,  Mabibi na Mabwana.

SHUKRANI
Kwanza napenda kumshukuru Mungu kwa baraka zake kwa kuweza kukutana tena mwaka huu tukiwa wenye afya njema.   Kipekee ninawashukuru wote mliohudhuria kwa kukubali mwaliko wetu ili tuweze kujumuika pamoja kusherekea siku hii ya wazazi na mahafali ya watoto wetu wa Chekechea  mwaka 2017. Kwa dakika chache naomba tusimame tuwakumbuke wazazi waliotutangulia mwaka huu wa 2017. 

Mkurugenzi wa Shule za Filbert Bayi, Anna Bayi.
HISTORIA YA  SHULE YA CHEKECHEA NA MSINGI
Mhe. Mgeni rasmi shule zetu za chekechea na msingi ziko katika makundi mawili kama ifuatavyo:-
i)  Kimara Dar es Salaam
    
Mwaka 1996 tulianzisha shule ya chekechea na msingi iliyopo Kimara na tulipata usajili mwaka   
    2000 kwa namba DS/02/7/007.  Mpaka sasa shule ina jumla ya wanafunzi 405 pia tunao waalimu     25 na wafanyakazi wasio waalimu 15

ii)  Mkuza-Kibaha
     Shule hii ilisajiliwa mwaka 2010 kwa namba PW.01/7/008.  Na ina jumla ya wanafunzi 290
     waalimu 17 na wafanyakazi wasio waalimu 10.

HISTORIA YA SHULE YA SEKONDARI
Mhe. Mgeni Rasmi Shule ya Sekondari Filbert Bayi yenye usajili wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi namba S.1377 na kituo cha Mitihani namba S.1437  ilianzishwa rasmi mwaka 2003 kule Kimara palipo Makao Makuu ya taasisi yetu na Kampasi ya shule ya Msingi.

Hatimaye majengo yalipokamilika Februari, 2004 tulihamia hapa Mkuza, Kibaha na kuzinduliwa na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya tatu Mhe.   Benjamin William Mkapa hapo tarehe 02/03/2005.

MAHAFALI YA CHEKECHEA
Ndugu  Mgeni Rasmi, Shule yetu ina utaratibu wa kufanya sherehe za mahafali ya wanafunzi wa Chekechea. Utaratibu huu ulianza mwaka 2006 na hii ni mahafali ya 12 kwa upande wa Kimara na 7 kwa Mkuza - Kibaha. 

Leo hii tunao jumla ya wanafunzi wa chekechea 71  kwa pande zote mbili Kimara na Mkuza ambao watapokea vyeti vyao vya kuhitimu Elimu hii ya awali. 

MAENDELEO YA SHULE
Ndugu Mgeni Rasmi shule zetu zina  mafanikio makubwa kitaaluma na michezo tangu zilipoanzishwa  kama ifuatavyo:-

i)  Shule za Chekechea 
Ndugu Mgeni Rasmi shule zetu za chekechea zinajitahidi sana katika taaluma ambapo wanafunzi wanaohitimu huingia darasa la kwanza na hatimaye kufika Sekondari.  Ni mategemeo yetu kuwa wanaohitimu leo hii wataendelea hadi watakapohitimu elimu ya msingi na sekondari.

ii)  Matokeo ya Mitihani - Msingi
Mwaka huu wa 2017, wanafunzi  63 wa darasa la saba walifanya mitihani ya Taifa na wamefaulu kwa asilimia (100%),  matokeo yao yanatuhakikishia watachaguliwa kwenda Sekondari.  Pia tunaamini wengi wao watarudi Shule yetu ya Sekondari,  kwani wanajua ubora na huduma za shule zetu. Tunawapongeza walimu wote wa darasa la saba kwa bidii na juhudi zao kubwa walizofanya kuhakikisha watoto wanafanya vizuri katika mitihani yao.

iii) Matokeo ya Mitihani - Sekondari
Mwaka 2016  wanafunzi  29 walifanya mtihani wa kidato cha nne na matokeo yao yalikuwa ni daraja la 1, 2 na 3 hakuna aliyepata daraja IV wala.

Tuna imani na matarajio makubwa zaidi ya haya kwa wanafunzi wetu waliomaliza kidato cha nne hivi karibuni nao watafanya vizuri kwa juhudi kubwa walizoonyesha Wanafunzi na Walimu  kwa ushirikiano na Wazazi.

SAFARI ZA KITAALUMA, MKOA WA IRINGA
Mhe. Mgeni Rasmi, shule zetu za Msingi na Sekondari zina utaratibu tuliojipangia wa kuwa na safari za kielimu kwa kutembelea  maeneo mbalimbali ya kihistoria ndani na nje ya nchi.  Mwezi Agosti mwaka huu  2017, Wanafunzi, Walimu na wafanyakazi wasio Walimu upande wa Sekondari walitembelea  Mkoa wa Iringa katika maeneo mbalimbali ya kihistoria kama vile Isimila, Mbuga za Wanyama za Ruaha, Kiwanda cha maziwa cha Asas nk.

MAZINGIRA
Ndg. Mgeni Rasmi Shule za Filbert Bayi zina utaratibu mahususi wa kutunza  MAZINGIRA ambapo  kila mwanafunzi hupewa mti na eneo la kutunza ikiwa ni zoezi endelevu hadi atakapoondoka shuleni kwetu ili ikamsaidie huko aendako kujua umuhimu wa kutunza mazingira.

ELIMU YA UJASIRIA MALI
Pamoja na masomo ya darasani, vijana wetu wanajifunza masomo ya ujasiriamali kama ufugaji wa kuku, upambaji wa kumbi kwa ajili ya sherehe mbalimbali, upishi, ususi, kunyoa, kupamba  maharusi na kutengeneza nywele. Taaluma hizi ninaamini zitawasaidia kuwa wajasiria mali wakati wamalizapo shule na vyuo.

SOBER HOUSE
Ndugu Mgeni Rasmi Taasisi ya Filbert Bayi inayo kituo kinachosaidia   watu walioathirika na Madawa ya Kulevya ambapo huwaweka kituoni kwa miezi minne kwa kuwafundisha na  kuwatibu, kuwapa ushauri nasaha , kuwajenga kiimani kwa kuwafundisha neno la Mungu na shughuli mbalimbali za Ujasiriamali.  Nashauri wazazi wenye ndugu au watoto wenye shida hiyo wawasiliane na ofisi ili wapewe maelekezo. Lakini pia wanaoguswa kusaidia mahitaji kwa waathirika hawa mf : Sabuni, mafuta na mavazi tunawakaribisha kufanya hivyo.

KITUO CHA AFYA
Taasisi ilianzisha Zahanati 2014 ambayo inasaidia wanafunzi na wananchi wengi wanaotuzunguka hapa shuleni na mwaka 2016 tulipandishwa hadhi na kuwa Kituo cha Afya.  Kituo chetu kinatoa huduma ya  vipimo mbalimbali ikiwemo upimaji Malaria, Ultra Sound, Full blood Picture, Cholestrol, Figo, Ini na vinginevyo.  Pia kituo kinatoa huduma ya mama na mtoto (RCH) ambazo zinatolewa bure lakini akinamama wanapojifungua huwa wanachangia gharama.

HITIMISHO
Ndugu Mgeni Rasmi tunakuomba utukamilishie siku hii kwa kutoa machache uliyonayo ikiwa ni pamoja na  kukamilisha sherehe zetu za Mahafali ya watoto wetu wa Chekechea na siku ya  Wazazi mwaka 2017 kwa kuwakabidhi Vyeti wahitimu na zawadi mbalimbali  kwa wanafunzi waliofanya vizuri kwenye masomo. 

ASANTENI KWA KUNISIKILIZA.

THE SPEECH OF THE GUEST OF HONOUR- FILBERT BAYI PRE-SCHOOL GRADUATION AND ANNUAL PARENTS DAY 25TH NOV 2017

Mkurugenzi Mkazi wa Unilever Tanzania, Akofa Ata.

Retired Major of the Armed Forces of Tanzania  Mr. Filbert Bayi

Executive Managing Director
Mrs Anna Bayi

Regional and Local Educational officers,

Members of Schools’ Board of Directors

School Committee members
Parents, invited guest, and students    
  
Mwenyekiti wa Shule za Filbert Bayi, Meja Mstaafu Filbert Bayi.
I would to take this opportunity to thank Mr. and Mrs. Bayi for inviting me to be a Guest of Honour on this very important and crucial day to witness Our Children the Pre-School pupils  graduating and the occasion of this year Annual Parents day Celebration.

I want to state that I have been very impressed by what the Chairman of the Board Mr. Filbert Bayi and The Managing Director Mrs. Anna Bayi  for setting up such huge and great investment , on Education , on Sports,  health facilities for both students and community surrounding the school. 

I have been also very impressed by the way the children did their presentation before us  here today expressing excellent intellectual performance.

I have also  witnessed very encouraging  confidence of the pupils and secondary students during their exhibition of their work, they have shown courage, good command of English language and competence of the subject matter. Your pupils and students have really done a good job to my observation, and of course we should appreciates teachers for that great work they are doing.

I should say that I was excited to hear the speech of the Managing Director on Academic performance of Filbert Bayi Pre-Primary, Primary and Secondary school  students. Parents and government should take note of such performance and encourage  such people like Mr. and Mrs. Bayi who are investing on education for our children.

It is natural that any good result demand a great preparation and command a huge cost. We should therefore appreciate that  the  Management of this school has really  created a good environment for learning for our pupils.

Employing of good and competent teachers must also be another factor which has contributed to such good performance. Such performance for standard seven, for Form two and Form four reflect a good picture of the school to the outsiders.

I would like to encourage the parents to continue supporting Mr. and Mrs. Bayi for a continued good work they are doing here.

Our Children and the society around us should appreciate for the additional  services provided here and make use of them such as Filbert Health Centre services in addition to Education services and many others.

Thank and may our good God strengthen you to continue serving our young generation our tomorrow leaders.

Thanks 

No comments:

Post a Comment