Friday 10 November 2017

DStv Kuonesha Tuzo za AFRIMA 2017

Na Mwandishi Wetu

WATEJA wa DStv wamepata nafasi ya kushuhudia Tuzo kubwa Afrika zinazotoa heshima na kutambua mchango wa wasanii kutoka Afrika,  kimataifa.

Ni Tuzo za AFRIMA (The All Africa Union Music Award Channel), ambazo zinatarajiwa kufanyika Jumapili hii na DStv imekuletea chaneli maalum kwa ajili ya kuonesha matukio yote muhimu na utoaji wa Tuzo hizi.

 Chaneli hii imeanza  kuanekana kuanzia Novemba 9 na inapatikana kwa wateja wote wa DStv kupitia namba 198 iliyopo kuanzia kifurushi Bomba cha sh.19,000 tu. Kwa kipindi cha siku tatu mfululizo,  wateja wa DStv watafurahia burudani kadha wa kadha kutoka kwa wasanii waliochaguliwa kwenye Tuzo hizi ikiwemo matamasha mbali mbali ya ndani na nje ya Bara  la Afrika kutoka kwa wasanii hawa.

Ni wakati wa watanzania  kushuhudia wasanii wetu wakipokea Tuzo zao za kimataifa  LIVE kupitia DStv pekee, Lipia Kifurushi chako cha DStv sasa kuanzia kifurushi Bomba kwa sh.19,000, ili usipitwe na Tuzo hizi.

 Majina ya wasanii kutoka Tanzania na vipengele walivyochaguliwa ni:

 Best Female Artist in Eastern Africa

Lady Jaydee – Sawa na Wao

Nandy- One Day

Feza Kessy - Walete

Vanessa Mdee- Cash Madame

 Best Male Artist in Eastern Africa

Ali Kiba – Aje

Diamond Platnumz – Eneka

 African Fans Favorite

Darassa- Muziki

 Best African Collaboration

Ali Kiba ft. MI – Aje

 Best Artiste/ Group in African Contemporary

Ali Kiba ft. MI – Aje

 Best Artist in African Pop

Diamond Platnumz- Eneka

 

Best Artist / Group in African R n B & Soul


Ali Kiba – Aje

No comments:

Post a Comment