Saturday 28 February 2015

Russia waandamana kupinga mauaji ya mpinzani



*Alikuwa akiandaa maandamano makubwa kumpinga Rais Putin


MOSCOW, Russia
MAELFU ya watu wanatarajia kushiriki katika maandamano makubwa katika mitaa ya jiji hili kuonesha heshima kwa mwanasiasa wa upinzani Boris Nemtsov, aliyeuawa kwa kupigwa risasi Ijumaa.
Mwanasiasa huo Jumapili alitarajia kuongoza maandamano makubwa, lakini wafuasi wake sasa watatumia maandamano hayo  kwa ajili ya kuomboleza kifo chake.
Rais wa Russia Vladimir Putin amelaani mauaji ya Bwana Nemtsov na kuahidi kuwa, Serikali yake itahakikisha wauaji wanapatikana.
Mauaji ya Bwana Nemtsov yanahusishwa na masuala ya kisiasa hasa kutokana na kumpinga Bwana Putin na ugomvi na Ukraine.
Wafuasi wa upinzani wanatarajia kuandamana Jumapili mchana katikati ya jiji la Moscow kabla ya kuelekea huko Great Moskvoretsky Bridge,ambako Bwana Nemtsov aliuawa.

Mamlaka ya jiji la Moscow awali waliidhinisha kuwa hadi watu 50,000 watashiriki katika maandamano hayo lakini waandaaji walisema kuwa watu zaidi wanawea kushiriki kushiriki kutokana na mauaji hayo.
Sarah Rainsford anasema kuwa mauaji hayo yameushtua upinzani wa Russia.
Katika eneo alilopigiwa risasi mpinzani huyo kumuwekwa lundo la mashada ya maua.
Watu wengi wanasema kuwa mauaji ya Boris Nemtsov yamefanyika kwa sababu za mtazamo wake kisiasa na wamemlamu rais Putin kwa tabia yake ya kupinga upinzani.
Nemtsov alizaliwa Oktoba 9 mwaka 1959 ni mwanasayansi na mwanasiasa na alifanikiwa sana kisiasa chini ya rais Boris Yeltsin katika miaka ya 1990, na tangu mwaka 2000 alikuwa akimkosoa Vladimir Putin.
Wakati akiuawa, Nemtsov alikuwa jijini Moscow akisaidia maandalizi ya mkutano wake mkubwa kwa ajili ya kupinga sera za rais Putin za kuiingiza Russia katika vita huko Ukraine na nchi hiyo kuwa katika matatizo ya fedha.

No comments:

Post a Comment