Tuesday 10 February 2015

Wapinzani wa Azam FC kutua Alhamisi


*Ni  wakali Al Merreikh ya Sudan


KIKOSI CHA Al Merreikh ya Sudan
Na Seba Nyanga
TIMU ya Al Merreikh ya Sudan Alhamisi Februari 12 inatarajia kutua jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kucheza na mabingwa wa Tanzania Bara Azam FC katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa Afrika.
Mchezo huo utafanyika mwishoni mwa wiki kwenye uwanja unaomilikiwa na mabingwa hao wa Bara wa Azam Complex uliopo Chamazi Mbagala.
Ofisa Habari wa Azam FC Jaffar Idd, alisema kuwa baada ya kuwasiri, miambao ambao ni mabingwa wa Kombe la Kagame watakutana na waandishi wa habari katika ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Azam FC wanaikumbuka Al Merreikh kwani walipokutana nao katika robo fainali ya Kombe la kagame huko Rwanda, matajiri hao wa azam walipokea kichapo na kutolewa kwa penati.
Idd alisema kuwa maandalizi ya mchezo huo yanaenda vizuri na timu hiyo kesho Jumatano itacheza na Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Azam FC walifungashwa virago na Mtibwa Sugar katika michuano ya Kombe la Mapinduzi huko kisiwani Zanzibar, hivyo Azam watataka kulipa kisasi katika mchezo huo wa kesho.

Vijana hao wa Azam FC ndio kwanza wamerejea nchini wakitokea Jamhuri ya Watu wa Kongo (DRC), ambako walijichimbia kwa siku kadhaa wakichza mechi mbalimbali ya kimataifa za kirafiki.

No comments:

Post a Comment