Tuesday 10 February 2015

Issa Hayatou kubadili Katiba CAF



 *Ataka aendelee kuwa rais


CAIRO, Misri
RAIS wa Shirikisho la Soka Afrika (Caf) Issa Hayatou anataka kubadili Katiba katika kipengere kinachohusu uko wa umri, ili aweze kugombea kipindi kingine tena cha uongozi.
Caf katika sheria zake inataka kiongozi aliyefikia umri wa miaka 70 kuachia ngazi lakini mabadiliko yatajadiliwa katika Mkutano Mkuu wa CAF mwezi Aprili.
Hayatou,mwenye umri wa miaka 68, anatumikia kipindi cha saba ofisini, baada ya kuchaguliwa kwa mara ya kwanza mwaka 1998.
"Fifa hawana ukomo wa umri kwa wajumbe wake wa Kamati ya Utendaji, hivyo Caf nao wanataka kutumia nafasi hiyo kubadili Katiba ili waende sambamba nao, alisema mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Caf Kwesi Nyantakyi.
Utawaka wa sasa wa Hayatou unamalizika mwaka 2017 na anasaka miaka mingine kinne ya kuliongoza shirikisho hilo la soka kwa miaka minne zaidi angalau hadi mwaka 2021, wakati atakaofikishaumri wa miaka 75.

Kipengere kimoja cha Katiba ya Caf kinasema hivi "wakati wa uchaguzi wao, wagombea wote lazima wawe wajumbe wa vyama vyao vya soka vya nchi wanazotoka, wagombea wote wa Kamati ya Utendaji ya Caf lazima wawe wajumbe wa Kamati ya Utendaji kwa vyama vyao vya soka vya nchi na lazimwawe na umri,

No comments:

Post a Comment