Wednesday 18 February 2015

Tanzania hoi Wavu wa Ufukweni

Mchezaji wa timu ya taifa ya Tanzania ya mpira wa wavu wa ufukweni Ismail Mohamed (kulia) akifanya vitu vyake walipocheza dhidi ya Kenya katika mchezo wa Kanda ya Tano Mikocheni Dar es Salaam jana. Tanzania ilifungwa 2-0.
Wachezaji wa timu ya taifa ya Tanzania Two, Hellen Richard (kulia) na Everlyne Alberth wakati wa mapumziko walipocheza na Kenya leo katika mchezo wa wavu wa ufukweni Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Wavu Tanzania (Tava) Agustino Agapa (kushoto) akimtibu mchezaji wa timu ya taifa Zuhura baada ya kuumia wakati wa mchezo wa Kanda ya tano ya Afrika dhidi ya Kenya.


Wachezaji wa timu ya Tanzania wakiwa pamoja na Wakenya baada ya mchezo wao leo.

Kocha wa timu ya wavu ya Tanzania Nasoro (kulia) akimsaidia mchezaji wake Zuhura baada ya kuumia alipocheza na Kenya.

Wachezaji wa timu za taifa za Kenya na Tanzania kabla ya kuanza kwa mchezo wao wa wavu wa ufukweni wa Kanda ya Tano ya Afrika.
Wachezaji wa timu ya Kenya Edna Rotch (kushoto) na Yunis Maiyo kabla ya kuanza kwa mchezo wao na Tanzania. Wakenya walishinda kwa seti 2-0.

No comments:

Post a Comment