Wednesday 11 February 2015

Azam FC yaishusha Yanga kileleni







Wachezaji wa Azam FC wakishangilia bao. (Picha na Maktaba)
Na Seba Nyanga
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara Azam FC, leo wamerejea kwa kishindo katika kilele cha msimamo wa ligi hiyo baada ya kuichapa Mtibwa sugar kwa bao 5-2 katika mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Chama Complex Mbagala Dar es Salaam.
Mabao mawili ya Frank Domayo na washambuliaji Kipre Tchetche na Didier Kavambagu, aliyefunga moja, yamewapa uongozi wa ligi hiyo Azam FC wakifikisha pointi 25 sawa na Yanga SC waliowafunga Mtibwa Sugar.
Mechi hiyo imeshuhudiwa na Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Mholanzi Mart Nooij aliyekuwa Jukwaa Kuu la Uwanja huo wakati Mtibwa Sugar ikipokea kipigo hicho cha aina yake.
Azam FC imefunga mabao 22 na kufungwa 12 wakati Yanga wamefunga mabao 15 na kuruhusu mabao saba.Kila timu imecheza jumla ya mechi 13.

Vikosi vilikuwa;
Azam FC: Manula, Kapombe, Nyoni/ Bocco (dk.65), Moradi, Wawa, Bolou/ Mudathir Yahya (dk. 55), Tchetche, Domayo, Kavumbagu/ Mcha (dk.80), Sure Boy na Majwega.

Mtibwa Sugar SC: Said Mohamed, Andrew Vicent, Majaliwa Mbaga, Ally Lundenga/ Vicent Barnabas (dk. 46), Salim Mbonde, Shaban Nditi, Ramadhani Kichuya, Musa Nampaka, Ame Ally Amour, Henry Joseph/ Ally Shomari (dk.33) na Musa Hassan Mgosi na / Abdallah Juma (dk. 70).

No comments:

Post a Comment