Monday 9 February 2015

Serekali yasimamisha ligi Misri



 *Ni baada ya vifo kutokea uwanjani sababu ya vurugu

 

Mashabiki wakizozana na polisi wakati wakitaka kuingia uwanjani.
CAIRO, Misri

SERIKALI ya Misri imesimamisha mechi za ligi kwa muda usiojulikana baada ya kutokea vurugu uwanjani na kusababisha vifo vya takribani watu 22.
Watu walipambana baada ya polisi kulipua mabomu ya machozi kwa mashabiki wa timu ya Zamalek waliokuwa wakilazimisha kuingia uwanjani kushuhudia mchezo dhidi ya wapinzani wao ENPPI.
Hatahivyo, mashabiki hao walilalamikia wahusika kwa kutumia mlango mmoja tu hapo uwanjani na kusababisha msongamano.
Hati ya kukamatwa imetolewa kwa viongozi wa kundi la mashabiki wa klabu ya Zamalek, ambao wanajulikana kama `the White Knights.
Kwa mara ya mwisho ligi ilisimamishwa mwaka 2012 baada ya mashabiki 74 kufa wakati wa vurug katika mchezo huko Port Said.
Angalau watu 20 waliumia Jumapili mjini hapa kwenye uwanja wa Jeshi la Anga, alisema shuhuda mmoja.
Licha ya vurugu hizo, mchezo huo uliendelea.
Uwanjani jozi za viatu viliachwa na watu waliouawa huku majeruhi wakiwa hoi uwanjani hapo.
Mashabiki wa Zamalek wanadai kuwa vurugu hizo zilianza wakati viongozi walipofungua geti moja la waya kuruhusu watu kuingia uwanjani.
Mashuhuda hao walisema kuwa ukuta wa waya ulianguka wakati umati wa watu ukilazimisha kuingia. "Mara askari walianza kulipua mabomu ya machozi," alisema shuhuda mmoja.

No comments:

Post a Comment