Friday 27 February 2015

Walimu Kinondoni waandaliwa kwa Umisseta



 *Lengo ni kuzalisha walimu wenye ujuzi watakaotoa wachezaji bora

Mratibu wa michezo mkoa wa Kinondoni Mwl. Samuel Robert akizungumza Makongo leo kabla ya ufungaji rasmi wa mafunzo ya walimu wa michezo wa shule za sekondari Kinondoni. 
Na Mwandishi Wetu
KANDA ya Kinondoni imekamilisha mafunzo maalum kwa ajili ya walimu wa shule za sekondari watakaofundisha mikoa yao kwa ajili ya kuiwezesha kanda hiyo kuendelea kutamba katika mashindano ya Michezo ya Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA).
Kinondoni kwa miaka minne mfuulizo imetamba katika Michezo ya Umisseta kwa kutwaa vikombe vingi na kuwa mshindi wa jumla wa mashindano hayo ya kila mwaka.
Mratibu wa michezo Kanda ya Kinondoni mwalimu Samuel Robert amesema leo kuwa, lengo la mafunzo hayo n
i kuzalisha walimu wenye ujuzi ili kutoa wanafunzi wenye uwezo katika michezo mbalimbali na kuiwezesha kanda yao kuendelea kufanya vizuri kitaifa.


Wakufunzi wa mafunzo ya riadha kwa baadhi ya walimu wa Kanda ya Kinondoni Suleiman Nyambui (kushoto aliyekaa) na Mwinga Mwanjala wakiwa katika picha ya pamoja na walimu hao baada ya kumaliza mafunzo hayo leo Makongo jijini Dar es Salaam.
Alisema mafunzo hayo yaliohusisha michezo mbalimbali pia yatasaidia kuongeza ari kwa walimu hao ili wafundishe kwa utaalam zaidi.
Mafunzo hayo ya siku tano yalishirikisha swalimu 30 kutoka shule mbalimbali za sekondari Kanda ya Kinondoni na yalihusu michezo ya mpira wa miguu, kikapu, wavu, netiboli, mpira wa mikono na riadha.
Alisema kuwa kila mchezo ulikuwa na walimu watano na ulifundishwa na wakufunzi walioletwa na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kupitia vyama au mashirikisho ya kitaifa ya michezo hiyo.
Mafunzo hayo yalitolewa na wataalam wa kitaifa na kimataifa wa michezo hapa nchini kama akina Suleiman Nyambui na Mwinga Mwanjala wa riadha, Manase Zablon wa kikapu na wengine.
Kanda ya Kinondoni kiumisseta wameigawa katika wilaya mbalimbali za Kawe, Ubungo, Wilaya Maalum ya Makongo na Kinondoni yenyewe.
Naye mkufunzi wa riadha Nyambui aliwataka walimu kuzingatia mafunzo hayo ili kuchagua wanafunzi wenye sifa watakaokuwa na uwezo wa kufanya vizuri katika mchezo wa riadha.


Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania (RT) Suleiman Nyambui (mbele) akisisitiza jambo kwa mmoja wa washiriki wa mafunzo ya siku tano ya michezo kwa walimu wa sekondari Mkoa wa Kinondoni. Kulia ni mkufunzi mwenzake Mwinga Mwanjala.

No comments:

Post a Comment